Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 8(1) (a); wananchi ndio chimbuko la mamlaka ya utawala wa nchi na kwamba Serikali itapata mamlaka kutoka kwao. Uchaguzi ndio namna pekee ya wananchi kukasimisha mamlaka yao kwa viongozi. Ni Haki ya kila raia kushiriki katika michakato ya Uchaguzi ikiwemo kupiga au kupigiwa kura kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi ili kupata viongozi.
Mtandao wa Uangalizi wa Uchaguzi Tanzania (TACCEO) na Jukwaa la Sera (Policy Forum) tumeendelea kufuatilia mchakato wa utayarishaji wa Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa,2019 nchini Tanzania kwa kutoa maoni kwenye rasimu ya kanuni husika
Asasi za Kiraia Wanachama wa TANGO, TUCTA na CCT na sekta ya AZAKI Tanzania inaitaka SADC kuchukua hatua za haraka juu ya Ukatili unaofanywa dhidi ya watu wa mataifa mengine nje ya nchini Afrika Kusini.
Wanachama wa mtandao wa Policy Forum wanaounda kikundi kazi cha bajeti (BWG) wameishauri serikali kuboresha sekta ya kilimo na ufugaji ili nchi iweze kufikia azimio lake la kuhakikisha inafikia uchumi wa kati wenye kuchagizwa na viwanda.
Ubalozi wa Uswisi hapa nchini kupitia Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi SDC umezindua awamu ya tatu ya programu ya uwajibikaji wa kijamii (Social Accountability Programme - SAP) ambayo inachangia kuziwezesha asasi za kiraia (AZAKI) zinazofany
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema imefurahishwa na kampeni ya Policy Forum iitwayo Stop the Bleeding ambayo inahusu udhibiti wa upotevu wa fedha za Umma kupitia njia haramu zikiwemo utakatishaji wa fedha na ukwepaji kodi.
Mwaka 2018 Policy Forum (PF) mtandao wa asasi zaidi ya 70 zilizosajiliwa Tanzania ilichapisha utafiti unaohusu mikataba ya utozaji kodi mara mbili (Double Taxation Agreements - DTAs) kati ya Tanzania na Afrika Kusini na Tanzania na India.
“Kufanikiwa Kuwa na Serikali Yenye Uwazi Kunahitaji Nchi Iweke Mifumo na Mipango Inayohitaji Kuakisiwa Katika Sera, Sheria na Taasisi za Taifa.” Jakaya Kikwete, 2013
Ufanisi wa mfumo wowote ule wa kukusanya kodi za majengo unahitaji ushirikiano imara kati ya Mamlaka ya Ukusanyaji wa Kodi na Halmashauri za Miji/Majiji. Aidha, ni budi kuwepo na mgawanyo ulio wazi na bayana wa majukumu na madaraka ya mamlaka hizo.