Skip to main content

Muhtasari wa Ripoti: Ukusanyaji wa Mapato ya Ndani Kwenye Sekta ya Uziduaji Unavyoweza Kufadhili Mabadiliko ya Tabianchi

Imechapishwa na Policy Forum

Kama ilivyo kwa nchi nyingi zinazoendelea, Tanzania imeathiriwa sana na mabadiliko ya tabianchi, madhara ambayo hayaishii tu kusababisha mafuriko na ukame lakini yanaharibu miundombinu na hata kuathiri maisha ya watanzania kwani kilimo, sekta inayoajiri watu wengi takriban asilimia 65.5 imeathiriwa sana na hali mbaya ya mvua. Aidha, athari za mabadiliko ya tabianchi pia zimeathiri sekta ya uziduaji hususan ufanisi katika shughuli za Uchimbaji mkubwa na mdogo wa madini (Large- & Small-scale mining operations).

Mwongozo wa Uanachama wa Policy Forum 2022

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum (PF) ni mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) yapatayo 60 ulionzishwa mwaka 2003 na kusajiliwa chini Sheria ya Mashirika yasiyo ya kiserikali ya mwaka 2002 ikiwa na usajili namba NGO/R2/00015. Policy Forum ina wanachama mbalimbali ambao hujumuika kwa pamoja wakiwa na malengo ya kushawishi michakato ya kisera ili kupunguza umasikini, kuongeza usawa na demokrasia; huku mkazo mkubwa ukiwekwa katika uwajibikaji kwenye matumizi ya fedha za umma katika ngazi ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa.

Mchango wa Redio ya Jamii katika Kutatua Changamoto za Afya, Newala

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum (PF) ni mtandao wenye muunganiko wa zaidi ya asasi za kiraia 60 ulioanzishwa mwaka 2003 kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanachama wa PF wana malengo ya kuhamasisha utungwaji wa sera zenye kulenga kupunguza umaskini, kuleta uwajibikaji katika fedha za umma kuanzia ngazi ya chini hadi Serikali Kuu.

Kufungwa kwa Ofisi kwa Ajili ya Sikukuu za Mwisho wa Mwaka

Imechapishwa na Policy Forum

Tunapenda kuwaataarifu wadau na wanachama wetu kwamba ofisi ya Sekretarieti ya Policy Forum itafungwa kwa ajili ya likizo ya Krismasi na Mwaka Mpya kuanzia tarehe 17 Disemba 2021 mpaka tarehe 9 Januari 2022.

 

Tunawatakia sikukuu njema za mwisho wa mwaka.

 

Tamisemi Kushirikiana na AZAKI kuandaa Mwongozo wa Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu Wenye Ulemavu

Imechapishwa na Policy Forum

Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017-2020/21), pamoja na malengo mengine, unakusudia kuweka mazingira wezeshi kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kimaendeleo kama vile uvuvi, kilimo, ufugaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.

Miongoni mwa mikakati iliyowekwa na Serikali ya kutimiza lengo la kusaidia makundi hayo ni utoaji wa mikopo isiyo na riba.

Kanuni za Utoaji wa Mikopo na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu za Mwaka 2019

Imechapishwa na Policy Forum

Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017-2020/21), pamoja na malengo mengine, unakusudia kuweka mazingira wezeshi kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kiuchumi kama vile kilimo, ufugaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.

Miongoni mwa mikakati ya kutimiza lengo hilo iliyoainishwa katika Mpango huo ni utoaji wa mikopo yenye gharama na masharti nafuu kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Zijue Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa: Ngazi ya Vijiji, Mitaa na Vitongoji, 2019

Imechapishwa na Policy Forum

 Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 8(1) (a); wananchi ndio chimbuko la mamlaka ya utawala wa nchi na kwamba Serikali itapata mamlaka kutoka kwao. Uchaguzi ndio namna pekee ya wananchi kukasimisha mamlaka yao kwa viongozi. Ni Haki ya kila raia kushiriki katika michakato ya Uchaguzi ikiwemo kupiga au kupigiwa kura kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi ili kupata viongozi.

Subscribe to Resources