Skip to main content

Midahalo ya Raia Makini Yafichua Mianya ya Uwajibikaji

Imechapishwa na Policy Forum

Midahalo ya umma iliyofanyika chini ya mradi wa Raia Makini imebainisha changamoto kubwa zinazowakabili wananchi katika upangaji na utekelezaji wa bajeti za serikali za mitaa, huku ikiongeza utayari wa wananchi kushirikiana na viongozi katika usimamizi wa rasilimali za umma. Midahalo hiyo imeonesha wazi kuwa wananchi wanapopewa taarifa sahihi na nafasi salama ya kujieleza, wako tayari kuuliza maswali, kudai uwajibikaji na kuchangia kwa njia chanya maendeleo ya maeneo yao.

Wananchi Wahimizwa Kuchukua Nafasi ya Uongozi Wahimizwa Kushiriki Katika Maamuzi ya Maendeleo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika

Imechapishwa na Policy Forum

Mdahalo wa wa asubuhi chini ya mradi wa Raia Makini ulifanyika tarehe 17 Novemba 2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, mkoani Katavi. Lengo kuu lilikuwa kuangazia umuhimu wa ushiriki wa wananchi katika upangaji wa mipango na bajeti, pamoja na namna Halmashauri inavyotarajia kuwawezesha wananchi kushiriki katika mchakato wa bajeti.

Vinara wa Uwajibikaji Wajengewa Uwezo Kuhusu Mfumo Ulioboreshwa wa O&OD na Mchakato wa Bajeti katika Ngazi ya Msingi

Imechapishwa na Policy Forum

 

Vinara wa Uwajibikaji (Community Accountability Champions – CACs) kutoka wilaya za Tanganyika mkoani Katavi na Mpwapwa mkoani Dodoma wamejengewa uwezo kupitia mafunzo maalum yaliyoratibiwa chini ya mradi wa Raia Makini, unaotekelezwa na Wajibu – Institute of Public Accountability kwa kushirikiana na Policy Forum, kwa ufadhili wa pamoja kutoka Umoja wa Ulaya (EU).

Muhtasari wa Ripoti: Ukusanyaji wa Mapato ya Ndani Kwenye Sekta ya Uziduaji Unavyoweza Kufadhili Mabadiliko ya Tabianchi

Imechapishwa na Policy Forum

Kama ilivyo kwa nchi nyingi zinazoendelea, Tanzania imeathiriwa sana na mabadiliko ya tabianchi, madhara ambayo hayaishii tu kusababisha mafuriko na ukame lakini yanaharibu miundombinu na hata kuathiri maisha ya watanzania kwani kilimo, sekta inayoajiri watu wengi takriban asilimia 65.5 imeathiriwa sana na hali mbaya ya mvua. Aidha, athari za mabadiliko ya tabianchi pia zimeathiri sekta ya uziduaji hususan ufanisi katika shughuli za Uchimbaji mkubwa na mdogo wa madini (Large- & Small-scale mining operations).

Mwongozo wa Uanachama wa Policy Forum 2022

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum (PF) ni mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) yapatayo 60 ulionzishwa mwaka 2003 na kusajiliwa chini Sheria ya Mashirika yasiyo ya kiserikali ya mwaka 2002 ikiwa na usajili namba NGO/R2/00015. Policy Forum ina wanachama mbalimbali ambao hujumuika kwa pamoja wakiwa na malengo ya kushawishi michakato ya kisera ili kupunguza umasikini, kuongeza usawa na demokrasia; huku mkazo mkubwa ukiwekwa katika uwajibikaji kwenye matumizi ya fedha za umma katika ngazi ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa.

Mchango wa Redio ya Jamii katika Kutatua Changamoto za Afya, Newala

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum (PF) ni mtandao wenye muunganiko wa zaidi ya asasi za kiraia 60 ulioanzishwa mwaka 2003 kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanachama wa PF wana malengo ya kuhamasisha utungwaji wa sera zenye kulenga kupunguza umaskini, kuleta uwajibikaji katika fedha za umma kuanzia ngazi ya chini hadi Serikali Kuu.

Subscribe to Resources