Midahalo ya Raia Makini Yafichua Mianya ya Uwajibikaji
Midahalo ya umma iliyofanyika chini ya mradi wa Raia Makini imebainisha changamoto kubwa zinazowakabili wananchi katika upangaji na utekelezaji wa bajeti za serikali za mitaa, huku ikiongeza utayari wa wananchi kushirikiana na viongozi katika usimamizi wa rasilimali za umma. Midahalo hiyo imeonesha wazi kuwa wananchi wanapopewa taarifa sahihi na nafasi salama ya kujieleza, wako tayari kuuliza maswali, kudai uwajibikaji na kuchangia kwa njia chanya maendeleo ya maeneo yao.