Mwongozo wa Uanachama wa Policy Forum 2022
Policy Forum (PF) ni mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) yapatayo 60 ulionzishwa mwaka 2003 na kusajiliwa chini Sheria ya Mashirika yasiyo ya kiserikali ya mwaka 2002 ikiwa na usajili namba NGO/R2/00015. Policy Forum ina wanachama mbalimbali ambao hujumuika kwa pamoja wakiwa na malengo ya kushawishi michakato ya kisera ili kupunguza umasikini, kuongeza usawa na demokrasia; huku mkazo mkubwa ukiwekwa katika uwajibikaji kwenye matumizi ya fedha za umma katika ngazi ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa.