
Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017-2020/21), pamoja na malengo mengine, unakusudia kuweka mazingira wezeshi kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kiuchumi kama vile kilimo, ufugaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.
Miongoni mwa mikakati ya kutimiza lengo hilo iliyoainishwa katika Mpango huo ni utoaji wa mikopo yenye gharama na masharti nafuu kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.