Skip to main content

Tamko Rasmi:-Bajeti 2015/2016

Imechapishwa na Policy Forum

Bajeti ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2015/16 kwa sasa inajadiliwa Bungeni. Bajeti nzima ya Serikali itawasilishwa na Waziri wa Fedha mara baada ya uwasilishaji na mjadala wa bajeti za wizara kukamilika. Kwa kuzingatia umuhimu wa tukio hili kitaifa, wajumbe wa  Kikundi Kazi cha  Bajeti cha Policy Forum, tunapenda kutoa mchango wetu katika mchakato huu muhimu kwa kuchangia uchambuzi wetu. 

Miswada Ya Takwimu Pamoja Na Makosa Ya Mtandao, 2015

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi, wanachama wa Policy Forum, Mtandao  wa mashirika yasiyo ya kiserikali, tuliokutana tarehe 29 na 30 Aprili, 2015 katika mkutano wetu wa mwaka (AGM) Dar es salaam, tumesoma na kuchambua kwa kina Miswada ya  Sheria ya Takwimu pamoja na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 kwa lengo la kujieleimisha na masuala ya katiba na uchaguzi mkuu 2015.

1.       SHERIA YA TAKWIMU NA SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAONI

Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka Wa Fedha 2014/15 Toleo La Bajeti Ya Wananchi

Imechapishwa na Policy Forum

Kijitabu cha Bajeti ya Serikali toleo la mwananchi kinatolewa kuboresha upatikanaji wa taarifa za kibajeti kwa lengo la kuongeza uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa fedha za umma. Kinaelezea bajeti ya Serikali kwa lugha rahisi, ikitoa dondoo za mambo muhimu kwenye bajeti na kuifanya kuwa rahisi kwa mtu wa kawaida kuielewa. Sera na mipango iliyomo katika bajeti ya Serikali huathiri maisha ya wananchi kwa namna tofaut itofauti, hivyo ni muhimu kwao kuitafakari kikamilifu maana yake.

Muswada wa Bajeti, 2014

Imechapishwa na Policy Forum

Muswada huu unapendekeza kutungwa kwa sheria ya bajeti kwa lengo la kuweka mfumo wa kisheria utakaosimamia mchakato wa bajeti ya serikali kuanzia uandaaji, uidhinishaji, utekelezaji, ufuatiliaji, tathmini na utoaji taarifa.

Ufisadi katika sekta ya umeme unapima uadilifu na uwajibikaji wa serikali ya Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Kufuatia kutolewa na kujadiliwa kwa taarifa ya  Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kuhusu Independent Power Tanzania Limited (IPTL)  Akaunti  ya Tegeta  ya Escrow (TEA) bungeni  na kilio cha umma kilichofuatia  kuhusu kufichuliwa kwa  ufisadi ambao haujawahi kuwapo wa aina  hiyo, Sisi, Asasi za Kiraia (AZAKI) tajwa hapo chini , tunapenda kuwasilisha msimamo wetu wa pamoja kuhusu utata wa suala hili.

Tamko kwa Umma:-Asasi za kiraia zapongeza juhudi ya serikali ya kuongeza mapato kutokana na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kupunguza misamaha ya kodi

Imechapishwa na Policy Forum

Jumuiko la asasi za kiraia zinazoshawishi haki katika kodi Tanzania, zimeipongeza serikali kwa kuandaa rasimu ya Muswada wa Kodi ya Ongezeko la Thamani wa mwaka 2014 na Muswada wa Uendeshaji wa Kodi wa mwaka 2014 wenye madhumuni ya kuelekeza uendeshaji wa kodi ya  Ongezeko la Thamani na kuunda muundo wa kisasa na wenye ufanisi wa uendeshaji wa kodi. 

Kuvuja kwa mkataba wa Statoil kunadhihirisha kuwa usiri unavunja imani

Imechapishwa na Policy Forum

Kufuatia ugunduzi wa  uhakika wa hivi karibuni wa gesi  asilia Tanzania, nchi imejitokeza kuwa na uwezekano mkubwa wa uzalishaji gesi kwa kiwango cha juu katika Afrika ya Mashariki, na kuleta hamasa miongoni mwa  wananchi, jumuiya za kiraia, na wanasiasa kuhusu  matarajio ya  rasilimali  hiyo kuchochea maendeleo ya taifa .  Serikali,  inaaminika,  imeanza mchakato  wa kuandaa sera na miundo ya kisheria zitakazosaidia usimamizi  wa  uchunguzi, uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa gesi asilia.

Subscribe to Resources