Skip to main content

Ufisadi katika sekta ya umeme unapima uadilifu na uwajibikaji wa serikali ya Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Kufuatia kutolewa na kujadiliwa kwa taarifa ya  Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kuhusu Independent Power Tanzania Limited (IPTL)  Akaunti  ya Tegeta  ya Escrow (TEA) bungeni  na kilio cha umma kilichofuatia  kuhusu kufichuliwa kwa  ufisadi ambao haujawahi kuwapo wa aina  hiyo, Sisi, Asasi za Kiraia (AZAKI) tajwa hapo chini , tunapenda kuwasilisha msimamo wetu wa pamoja kuhusu utata wa suala hili.

Tamko kwa Umma:-Asasi za kiraia zapongeza juhudi ya serikali ya kuongeza mapato kutokana na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kupunguza misamaha ya kodi

Imechapishwa na Policy Forum

Jumuiko la asasi za kiraia zinazoshawishi haki katika kodi Tanzania, zimeipongeza serikali kwa kuandaa rasimu ya Muswada wa Kodi ya Ongezeko la Thamani wa mwaka 2014 na Muswada wa Uendeshaji wa Kodi wa mwaka 2014 wenye madhumuni ya kuelekeza uendeshaji wa kodi ya  Ongezeko la Thamani na kuunda muundo wa kisasa na wenye ufanisi wa uendeshaji wa kodi. 

Kuvuja kwa mkataba wa Statoil kunadhihirisha kuwa usiri unavunja imani

Imechapishwa na Policy Forum

Kufuatia ugunduzi wa  uhakika wa hivi karibuni wa gesi  asilia Tanzania, nchi imejitokeza kuwa na uwezekano mkubwa wa uzalishaji gesi kwa kiwango cha juu katika Afrika ya Mashariki, na kuleta hamasa miongoni mwa  wananchi, jumuiya za kiraia, na wanasiasa kuhusu  matarajio ya  rasilimali  hiyo kuchochea maendeleo ya taifa .  Serikali,  inaaminika,  imeanza mchakato  wa kuandaa sera na miundo ya kisheria zitakazosaidia usimamizi  wa  uchunguzi, uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa gesi asilia.

Tamko la Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi wajumbe wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum, tunaowakilisha zaidi ya Asasi  70 za Kiraia tuliounganisha nguvu zetu  ili kuchangia katika kuifanya michakato ya sera ngazi ya serikali za mitaa kuwa yenye uwazi zaidi, ya kidemokrasia, iliyo shirikishi na yenye uwajibikaji, tunapenda kutoa  mchango wetu katika mchakato huu  muhimu wa uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2014.  

Tamko la Kikundi Kazi cha Bajeti Kuhusiana na Bajeti ya Mwaka 2014/15

Imechapishwa na Policy Forum

Wakati Waziri wa Fedha  anapowasilisha  Bajeti ya Taifa  kwa mwaka wa Fedha 2014/15  Bungeni  kesho, sisi  Wajumbe wa  Kikundi Kazi cha Bajeti  cha  Policy Forum, tunaowakilisha zaidi ya Asasi  70 za Kiraia tuliounganisha nguvu zetu  ili kuongeza uelewa na  ushiriki wa jamii katika uandaaji wa sera, tunapenda kutoa  mchango wetu katika mchakato huu  muhimu.   

Mdahalo wa Asubuhi wa Policy Forum wa Jinsi ya Kufaidika na Gesi:Jinsi ya Kuimarisha Ushiriki wa Wananchi Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Pamoja na kupatikana  na hifadhi ya gesi Tanzania , kumekuwa na majadiliano wa kutosha ya jinsi  uchimbaji wa rasilimali hii unaweza kuboreshwa ili  uweze kuwanufaisha wananchi nchini . Wadau wametoa wito kwa Serikali kuonyesha dhamira itakayoweza kuelekea kuimarisha ushiriki wa wananchi (local content) katika sekta ya madini na makampuni ya mafuta na gesi ya kimataifa kuonyesha hatua madhubuti itakazochukua juu ya hili ikiwa ni pamoja na maendeleo ya rasilimali watu .

Subscribe to Resources