Ufisadi katika sekta ya umeme unapima uadilifu na uwajibikaji wa serikali ya Tanzania
Kufuatia kutolewa na kujadiliwa kwa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kuhusu Independent Power Tanzania Limited (IPTL) Akaunti ya Tegeta ya Escrow (TEA) bungeni na kilio cha umma kilichofuatia kuhusu kufichuliwa kwa ufisadi ambao haujawahi kuwapo wa aina hiyo, Sisi, Asasi za Kiraia (AZAKI) tajwa hapo chini , tunapenda kuwasilisha msimamo wetu wa pamoja kuhusu utata wa suala hili.