Skip to main content

Sekta ya Kilimo na Mifugo Yatajwa Kama Chachu ya Kufikia Uchumi wa Viwanda

Imechapishwa na Policy Forum

Wanachama wa mtandao wa Policy Forum wanaounda kikundi kazi cha bajeti (BWG) wameishauri serikali kuboresha sekta ya kilimo na ufugaji ili nchi iweze kufikia azimio lake la kuhakikisha inafikia uchumi wa kati wenye kuchagizwa na viwanda. Hayo yamesemwa tarehe 4 Mei 2019 Jijini Dodoma ambapo wanachama hao walikutana na wabunge wa kamati ya bajeti na mtandao wa kupambana na rushwa wa afrika tawi la Tanzania (APNAC-TANZANIA).

Uswisi kushirikiana na Tanzania kuimarisha uwajibikaji

Imechapishwa na Policy Forum

Ubalozi wa Uswisi hapa nchini kupitia Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi SDC umezindua awamu ya tatu ya programu ya uwajibikaji wa kijamii (Social Accountability Programme - SAP) ambayo inachangia kuziwezesha asasi za kiraia (AZAKI) zinazofanya kazi ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania.

Tamko La Policy Forum Na Wadau Wengine Juu Ya; Mapendekezo Ya Kuboresha Sheria Ya Takwimu

Imechapishwa na Policy Forum

Kufuatia kupitishwa kwa sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2018,  Sisi wadau kutoka Asasi za Kiraia na watafutaji, watumiaji na wasambazaji wa taarifa za takwimu tumekutana kufanya uchambuzi wa kina wa sheria hii;

Pamoja na kutambua umuhimu wa sheria hii ambayo imelenga kuzuia usambazaji/ uchapishaji wa taarifa za kitakwimu zinazoweza kupotosha umma;

Mkurugenzi wa TAKUKURU Afurahishwa na Kampeni ya Kudhibiti Upotevu wa Fedha za Umma

Imechapishwa na Policy Forum

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema imefurahishwa na kampeni ya Policy Forum iitwayo Stop the Bleeding ambayo inahusu udhibiti wa upotevu wa fedha za Umma kupitia njia haramu zikiwemo utakatishaji wa fedha na ukwepaji kodi. Hayo yamesemwa Novemba 11, 2018 Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Diwani Athumani alipokuwa akiongea na Wabunge wa Bunge Tanzania Wanaopamba na Rushwa (APNAC).

Mikataba ya utozaji kodi mara mbili (DTAs) na hatma yake kwa nchi

Imechapishwa na Policy Forum

Mwaka 2018 Policy Forum (PF) mtandao wa asasi zaidi ya 70 zilizosajiliwa Tanzania ilichapisha utafiti unaohusu mikataba ya utozaji kodi mara mbili (Double Taxation Agreements - DTAs) kati ya Tanzania na Afrika Kusini na Tanzania na India. Makala hii ni tafsiri ya muhtasari wa utafiti huo ambao ulitumika kwenye kikao cha pamoja na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao wapo kwenye Mtandao wa Kupambana na Rushwa (APNAC) mnamo Novemba 8, 2018 Jijini Dodoma.

Utozaji Kodi kwa Miji Inayokuwa Tanzania: Ukusanyaji wa Kodi ya Majengo kati ya Serikali Kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa

Imechapishwa na Policy Forum

Ufanisi wa mfumo wowote ule wa kukusanya kodi za majengo unahitaji ushirikiano imara kati ya Mamlaka ya Ukusanyaji wa Kodi na Halmashauri za Miji/Majiji. Aidha, ni budi kuwepo na mgawanyo ulio wazi na bayana wa majukumu na madaraka ya mamlaka hizo. Katika miaka kumi iliyopita mfumo wa kukusanya kodi ya majengo katika Tanzania umekuwa ukibadilika mara kwa mara kati ya mfumo wa kugatua madaraka kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mfumo wa kukusanya kodi hiyo moja kwa moja kwa kutumia Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi ya Serikaali Kuu.

Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari: Maoni Ya Kikundi Kazi Cha Bajeti Cha Policy Forum Kuhusu Bajeti Ya Taifa 2018/2019

Imechapishwa na Policy Forum

Dodoma, Julai 17 2018

Tarehe 14 mwezi wa Juni 2018 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Philip Mpango aliwasilisha Bungeni Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2018/19 kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa na Bunge ili kuruhusu utekelezaji wake ifikapo Julai Mosi 2018. Hotuba hii ya Waziri ilitanguliwa na mawasilisho ya bajeti za Wizara mbalimbali pamoja na mijadala.

Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP II): Ni kwa Jinsi Gani Tutaboresha Utekelezaji Katika Mamlaka ya Serikali za Mtaa?

Imechapishwa na Policy Forum

Mwanzoni mwa mwaka 2016, Serikali ilizindua FYDP II, kwa lengo la kurekebisha mapungufu ya FYDP I na kutoa mpango makini wakati Tanzania inapoanza kuelekea katika maendeleo ya viwanda katika miaka mitano ijayo (2016 – 2021).

Katika kufanya marejeo ya FYDP I, serikali ilitambua kuwa mpango wa awali ulishindwa kufanikisha malengo yake mengi. Wakati Serikali imedhamiria kuwa ukuzaji wa viwanda ni kipaumbele katika miaka mitano ijayo, mapungufu ndani ya mpango unaweza kufanya nchi ishindwe kwa mara nyingine tena kama masuala yaliyojitokeza hayajafanyiwa kazi vya kutosha.

Subscribe to Resources