Skip to main content

Kikundi Kazi Cha Policy Forum Na Or-Tamisemi Wajadiliana Jinsi Ya Kuboresha Utendaji Katika Ngazi Za Serikali Za Mitaa Nchini

Imechapishwa na Policy Forum

Halmashauri nchini zimeshauriwa kubuni vyanzo vipya vya mapato ili ziweze kupata mapato ambayo yatasaidia katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo katika ngazi ya serikali za mitaa. Hayo yamesemwa Oktoba 27, 2017 mjini Dodoma na wawakilishi wa idara mbalimbali za Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) wakati wa mkutano uliojumuisha wanachama wa Policy Forum (PF) na maafisa wa OR-TAMISEMI.

Ripoti Fupi Ya Uchambuzi Wa Bajeti Ya Wizara Ya Nishati Na Madini Kwa Mwaka 2017/2018

Imechapishwa na Policy Forum

Sekta ya nishati inakabiliwa na changamoto mbalimbali hapa nchini ikiwemo: upungufu wa fedha za kutosha, ushiriki na uwekezaji mdogo wa sekta binafsi katika miradi mikubwa ya nishati; utegemezi mkubwa sana kwa tungamotaka kama chanzo cha nishati; gharama kubwa za tozo za uunganishaji na usambazaji wa umeme; upungufu wa wataalam na tafiti; uwepo na matumizi ya teknolojia miundombinu duni; na uwekezaji mdogo katika nishati jadidifu. Soma zaidi...

Uchambuzi Wa Utekelezaji Wa Mapato Na Matumizi Ya Mwaka 2016/2017 Na Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Kwa Mwaka 2017/2018

Imechapishwa na Policy Forum

Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni sekta muhimu sana kwa uchumi na maendeleo ya nchi na Watanzania
kiujumla. Sekta hizi zimeendelea kuwa chanzo kikubwa cha kipato kwa zaidi ya asilimia 65 ya
Watanzania na nguzo muhimu katika kuhakikisha usalama wa chakula, na zinachangia pato la taifa
kwa zaidi ya asilimia 29 na kwa mauzo ya nje zinachangia kwa zaidi ya asilimia 24.

Viwango vya Utawala Bora na Usimamizi wa Rasilimali Asilia (RGI) hutathmini jinsi nchi zenye utajiri wa rasilimali za Mafuta, Gesi na Madini zinavyojisimamia

Imechapishwa na Policy Forum

Sekta ya Mafuta na Gesi asilia ina alama 53 kati ya alama 100 za RGI 2017. Tofauti na sekta ya madini ambayo ni kongwe, Tanzania bado haijaanza uzalishaji mkubwa wa gesi baada ya ugunduzi wa gesi nyingi katika kina kirefucha bahari ya Hindi  ambayo hivi sasa inakadiriwa kuwa futi za ujazo trilioni 57. Hali ya kuridhisha ya Tanzania katika uwezekano wa kupata thamani ya rasilimali, kipengele kinachopima ubora wa utawala katika utoaji wa leseni, mfumo wa kodi, athari kwa jamii na ushiriki wa Serikali, hutegemea sana utaratibu wa kisheria wenye masharti mahimu kuhusu utawala na uwazi.

Mapitio ya " Suala la Dola Bilioni Moja": Tanzania Inaendelea Kupoteza Kiasi Gani cha Fedha za Kodi?

Imechapishwa na Policy Forum

Serikali inalo jukumu kubwa la kuwahakikishia na kuwapatia watu wake huduma na bidhaa za umma. Hizi ni pamoja na afya, elimu, maji, miundombinu, ulinzi na usalama na kadhalika. Huduma na bidhaa hizi ni muhimu sana ili wananchi waweze kustawi na kuondokana na matatizo kama vile umaskini, ujinga na maradhi.Huduma na bidhaa za umma hugharimu rasilimali nyingi zikiwemo fedha. Fedha hizi ni za kutoka ndani na nje ya nchi. Fedha za ndani ni pamoja na mapato ya kikodi na yasiyo ya kikodi.

Kuelekea Uwajibikaji Endelevu Katika Usimamizi Wa Maliasili Nchini Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Siku chache zilizopita, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli aliunda kamati mbili za wataalamu kwa ajili ya kuchunguza taarifa za kuwapo kwa udanganyifu wa kiwango cha madini katika mchanga wa dhahabu (makinikia), ambao umekuwa ukisafirishwa kupelekwa nje ya nchi. Mchanga huo ni ule unaotoka katika migodi ya dhahabu ya Bulyanhulu na Buzwagi ambayo kwa pamoja inamilikiwa na Kampuni ya Acacia.

Taarifa kwa Vyombo Vya Habari: Uzinduzi wa Ripoti ya Hali ya Utekelezaji wa Dira ya Madini ya Afrika

Imechapishwa na Policy Forum

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UZINDUZI WA RIPOTI YA HALI YA UTEKELEZAJI WA DIRA YA MADINI YA AFRIKA

Policy Forum kwa kushirikiana na Tax Justice Network – Africa (TNJ-A), Tanzania Tax Justice Coalition (TTJC) na HakiRasilimali wameandaa uzinduzi wa kitaifa wa Ripoti ya Hali ya Utekelezaji wa Dira ya Madini ya Afrika (AMV) utakaofanyika katika ukumbi wa Bunge (Old Dispensary Hall), Dodoma  tarehe 15 Mei, 2017.  Uzinduzi  huo utaanza saa 6:30 mchana.

Maelezo ya Ripoti ya Mbeki Kuhusu Uhamishaji Haramu wa Fedha kutoka Barani Afrika

Imechapishwa na Policy Forum

Februari 2015 Jopo la Ngazi ya Juu Kuhusu Uhamishaji Haramu wa Fedha kutoka Barani Afrika, likiongozwa na Mwenyekiti wake Rais Thabo Mbeki, liliwasilisha ripoti yake kwa Tume ya Umoja wa Afrika/Tume ya Umoja wa Kimataifa ya Kiuchumi Barani Afrika (AUC/ECA). Ripoti ilionesha kuwa nchi za Kiafrika hupoteza kwa wastani dola bilioni 50 kwa mwaka kutokana na uhamishaji haramu wa fedha. Shughuli za kibiashara za sekta binafsi ndizo zinazochangia kwa kiwango kikubwa uhamishaji haramu wa fedha (IFFs), zikifuatiliwa na uhalifu uliopangwa, kisha shughuli za sekta ya umma.

Subscribe to Resources