Skip to main content

Tamko la Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi wajumbe wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum, tunaowakilisha zaidi ya Asasi  70 za Kiraia tuliounganisha nguvu zetu  ili kuchangia katika kuifanya michakato ya sera ngazi ya serikali za mitaa kuwa yenye uwazi zaidi, ya kidemokrasia, iliyo shirikishi na yenye uwajibikaji, tunapenda kutoa  mchango wetu katika mchakato huu  muhimu wa uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2014.  

Tamko la Kikundi Kazi cha Bajeti Kuhusiana na Bajeti ya Mwaka 2014/15

Imechapishwa na Policy Forum

Wakati Waziri wa Fedha  anapowasilisha  Bajeti ya Taifa  kwa mwaka wa Fedha 2014/15  Bungeni  kesho, sisi  Wajumbe wa  Kikundi Kazi cha Bajeti  cha  Policy Forum, tunaowakilisha zaidi ya Asasi  70 za Kiraia tuliounganisha nguvu zetu  ili kuongeza uelewa na  ushiriki wa jamii katika uandaaji wa sera, tunapenda kutoa  mchango wetu katika mchakato huu  muhimu.   

Mdahalo wa Asubuhi wa Policy Forum wa Jinsi ya Kufaidika na Gesi:Jinsi ya Kuimarisha Ushiriki wa Wananchi Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Pamoja na kupatikana  na hifadhi ya gesi Tanzania , kumekuwa na majadiliano wa kutosha ya jinsi  uchimbaji wa rasilimali hii unaweza kuboreshwa ili  uweze kuwanufaisha wananchi nchini . Wadau wametoa wito kwa Serikali kuonyesha dhamira itakayoweza kuelekea kuimarisha ushiriki wa wananchi (local content) katika sekta ya madini na makampuni ya mafuta na gesi ya kimataifa kuonyesha hatua madhubuti itakazochukua juu ya hili ikiwa ni pamoja na maendeleo ya rasilimali watu .

Warsha ya Asasi za Kiraia Juu ya Viwango Vipya vya Mpango wa Uwazi wa Tasnia ya Uziduaji (EITI)

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum kwa kushirikiana na Mpango wa Uhamasishaji Uwazi katika Mapato ya Madini, Gesi asilia na Mafuta Tanzania ( TEITI ) pamoja na Hakimadini wameandaa warsha ( 2-3 Aprili 2014) Arusha kwa lengo la kuwawezesha wawakilishi wa asasi za kiraia za kaskazini mwa Tanzania zinazofanya kazi katika masuala ya uziduaji kuongeza uelewa wao wa viwango vipya vya  Mpango wa Uhamasishaji Uwazi katika Mapato ya Madini au Mpango wa Uwazi katika Tasnia ya Uziduaji (EITI) ili kuongeza uwezo wao wa kuiwajibisha serikali yao.

Subscribe to Resources