Tamko la Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014
Sisi wajumbe wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum, tunaowakilisha zaidi ya Asasi 70 za Kiraia tuliounganisha nguvu zetu ili kuchangia katika kuifanya michakato ya sera ngazi ya serikali za mitaa kuwa yenye uwazi zaidi, ya kidemokrasia, iliyo shirikishi na yenye uwajibikaji, tunapenda kutoa mchango wetu katika mchakato huu muhimu wa uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2014.