Skip to main content

Mjue Diwani (Toleo la Pili)

Imechapishwa na Policy Forum

Ndugu msomaji, tunayo furaha kukuletea kitabu kipya kiitwacho “Mjue Diwani”  ikiwa ni mwendelezo wa mkakati wetu wa kikundi kazi cha serikali za mitaa wa kuwaelimisha wananchi kuhusu utawala wa Serikali za Mitaa na kukuza uwajibikaji katika jamii. Kusoma zaidi bofya hapa

Tamko La Asasi Za Kiraia Kuhusu Viashiria Vya Uvunjifu Wa Amani Wiki Moja Kuelekea Tarehe Ya Upigaji Kura Katika Uchaguzi Mkuu Tanzania Tarehe 25.10.2015

Imechapishwa na Policy Forum

Asasi za Tanzania tumeendelea kufuatilia mchakato wa uchaguzi mkuu 2015 tangu uandikishaji wapiga kura, uhamasishaji hadi kampeni zinazoendelea kwa umakini mkubwa. AZAKI tumefanya hivyo tukiamini kuwa uchaguzi  ni sehemu kuu ya michakato ya kidemokrasia hapa nchini kama ilivyo duniani kote. Sisi asasi za kiraia Tanzania, tukiwa watetezi na wasimamizi wa demokrasia, utawala bora na haki za binadamu, hatumuungi mkono mgombea yeyote wala chama chochote cha kisiasa kinachotafuta kuingia madarakani wala hatulengi kuchukua dola.

Maswali Yetu Muhimu kwa Serikali ya Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Mfumo wa Uongozi / utawala wa sasa wa Tanzania utafikia mwisho wake katika miezi michache ijayo. Hii inatoa njia kwa mfumo mpya kuchukua hatamu ikitegemewa kuwa na mikakati mipya au iliyoboreshwa kusukuma maendeleo ya kiuchumi.

Makosa ya Rushwa Katika Chaguzi Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) tunakuletea tena chapisho hili la tatu katika mtiririko wa machapisho yanayohusu elimu kwa umma juu ya kupambana na rushwa.
Mtakumbuka kuwa chapisho letu la kwanza la pamoja lilihusu sheria mpya namba 11 ya mwaka 2007 ya kuzuia na kupambana na rushwa hapa Tanzania,

Chapisho hili linaweka wazi sheria zetu zinavyosema kuhusu makosa yarushwa katika chaguzi hapa nchini Tanzania na adhabu zinazotolewa kwa makosa husika,

Masuala Ya Wananchi Katika Katiba Inayopendekezwa: Uchambuzi Linganifu Kuhusu Yaliyomo Katika Katiba Inayopendekezwa, Rasimu Ya Katiba Ya Tume Ya Mabadiliko Ya Katiba Na Katiba Ya Jamhuri Ya Muungano Ya Mwaka 1977

Imechapishwa na Policy Forum

Kazi hii na nyingine nyingi zilizofanyika katika Mwaka 2014 zisingefanikiwa bila michango ya kiufundi, mawazo, maoni, ushauri, hali na mali kutoka kwa wadau, marafi ki na wawezeshaji mbalimbali. Ni jambo la kheri kuwa miaka minne ya maisha ya JUKWAA LA KATIBA TANZANIA imekuwa ya harakati, kazi na mafanikio makubwa kiasi hiki. Shukrani na pongezi nyingi ziwaendee wote walioamua kufanya kazi bega kwa bega na JUKATA kwa miaka yote tangu kuanzishwa rasmi kwa JUKATA na hasa katika mwaka wa 2014 hadi kukamilisha Kijitabu hiki

muhimu.

Utawala wa Kidemokrasia Katika Jamii (Toleo la 8)

Imechapishwa na Policy Forum

UTANGULIZI

Mwananchi ana wajibu na majukumu yake kuhakikisha kuwa Kiongozi aliyemchagua au kuteuliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo katika viwango vinavyokubalika katika eneo la kijiji/mtaa kulingana na mipango na makubaliano ya vikao vya kisheria vya kijiji na mtaa. Kila mwananchi ana wajibu wa kupinga na kukataa kila aina ya uovu katika jamii ikiwemo rushwa, uonevu, wizi, ubadhirifu wa mali za umma na ya watu binafsi.

Kampeni ya kupambana na utoroshwaji haramu wa rasilimali na fedha barani Afrika

Imechapishwa na Policy Forum

Tarehe 25 Juni 2015, Policy Forum ilishiriki kwenye uzinduzi wa kampeni “Stop The Bleeding” inayolenga kupambana na utoroshwaji haramu wa rasilimali na fedha barani Afrika. Kampeni hii ambayo inaongozwa na asasi za kiraia za kiafrika kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali ya kimataifa, inaazimia kufanyia kazi matokeo ya utafiti na mapendekezo ya ripoti ya Thabo Mbeki ijulikanayo kama "the High Level Panel on Illicit Financial Flows from Africa" ambayo imechunguza tatizo la utoroshwaji wa fedha hizi.

Miswada Kuhusu Tasnia Ya Uziduaji: Msimamo Wa Kikundi Kazi Cha Azaki Zinazoshiriki Kwenye Tasnia Ya Uziduaji

Imechapishwa na Policy Forum

Tarehe 16 Juni 2015 Serikali ya Tanzania  ilipeleka miswada mitatu bungeni inayohusu sekta ya uziduaji chini ya “Hati ya Dharura.”  Miswada hiyo ni Sheria ya Uwazi na Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia ya mwaka 2015 (The Tanzania Extractive Industries (Transparency and Accountability) Act 2015, Sheria ya Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesi ya mwaka 2015. (The Oil and Gas Revenue Management Act 2015)  Sheria ya Petroli ya mwaka 2015 (The Petroleum Act 2015).

Subscribe to Resources