Skip to main content

Masuala Ya Wananchi Katika Katiba Inayopendekezwa: Uchambuzi Linganifu Kuhusu Yaliyomo Katika Katiba Inayopendekezwa, Rasimu Ya Katiba Ya Tume Ya Mabadiliko Ya Katiba Na Katiba Ya Jamhuri Ya Muungano Ya Mwaka 1977

Imechapishwa na Policy Forum

Kazi hii na nyingine nyingi zilizofanyika katika Mwaka 2014 zisingefanikiwa bila michango ya kiufundi, mawazo, maoni, ushauri, hali na mali kutoka kwa wadau, marafi ki na wawezeshaji mbalimbali. Ni jambo la kheri kuwa miaka minne ya maisha ya JUKWAA LA KATIBA TANZANIA imekuwa ya harakati, kazi na mafanikio makubwa kiasi hiki. Shukrani na pongezi nyingi ziwaendee wote walioamua kufanya kazi bega kwa bega na JUKATA kwa miaka yote tangu kuanzishwa rasmi kwa JUKATA na hasa katika mwaka wa 2014 hadi kukamilisha Kijitabu hiki

muhimu.

Utawala wa Kidemokrasia Katika Jamii (Toleo la 8)

Imechapishwa na Policy Forum

UTANGULIZI

Mwananchi ana wajibu na majukumu yake kuhakikisha kuwa Kiongozi aliyemchagua au kuteuliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo katika viwango vinavyokubalika katika eneo la kijiji/mtaa kulingana na mipango na makubaliano ya vikao vya kisheria vya kijiji na mtaa. Kila mwananchi ana wajibu wa kupinga na kukataa kila aina ya uovu katika jamii ikiwemo rushwa, uonevu, wizi, ubadhirifu wa mali za umma na ya watu binafsi.

Kampeni ya kupambana na utoroshwaji haramu wa rasilimali na fedha barani Afrika

Imechapishwa na Policy Forum

Tarehe 25 Juni 2015, Policy Forum ilishiriki kwenye uzinduzi wa kampeni “Stop The Bleeding” inayolenga kupambana na utoroshwaji haramu wa rasilimali na fedha barani Afrika. Kampeni hii ambayo inaongozwa na asasi za kiraia za kiafrika kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali ya kimataifa, inaazimia kufanyia kazi matokeo ya utafiti na mapendekezo ya ripoti ya Thabo Mbeki ijulikanayo kama "the High Level Panel on Illicit Financial Flows from Africa" ambayo imechunguza tatizo la utoroshwaji wa fedha hizi.

Miswada Kuhusu Tasnia Ya Uziduaji: Msimamo Wa Kikundi Kazi Cha Azaki Zinazoshiriki Kwenye Tasnia Ya Uziduaji

Imechapishwa na Policy Forum

Tarehe 16 Juni 2015 Serikali ya Tanzania  ilipeleka miswada mitatu bungeni inayohusu sekta ya uziduaji chini ya “Hati ya Dharura.”  Miswada hiyo ni Sheria ya Uwazi na Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia ya mwaka 2015 (The Tanzania Extractive Industries (Transparency and Accountability) Act 2015, Sheria ya Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesi ya mwaka 2015. (The Oil and Gas Revenue Management Act 2015)  Sheria ya Petroli ya mwaka 2015 (The Petroleum Act 2015).

Tamko Rasmi:-Bajeti 2015/2016

Imechapishwa na Policy Forum

Bajeti ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2015/16 kwa sasa inajadiliwa Bungeni. Bajeti nzima ya Serikali itawasilishwa na Waziri wa Fedha mara baada ya uwasilishaji na mjadala wa bajeti za wizara kukamilika. Kwa kuzingatia umuhimu wa tukio hili kitaifa, wajumbe wa  Kikundi Kazi cha  Bajeti cha Policy Forum, tunapenda kutoa mchango wetu katika mchakato huu muhimu kwa kuchangia uchambuzi wetu. 

Miswada Ya Takwimu Pamoja Na Makosa Ya Mtandao, 2015

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi, wanachama wa Policy Forum, Mtandao  wa mashirika yasiyo ya kiserikali, tuliokutana tarehe 29 na 30 Aprili, 2015 katika mkutano wetu wa mwaka (AGM) Dar es salaam, tumesoma na kuchambua kwa kina Miswada ya  Sheria ya Takwimu pamoja na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 kwa lengo la kujieleimisha na masuala ya katiba na uchaguzi mkuu 2015.

1.       SHERIA YA TAKWIMU NA SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAONI

Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka Wa Fedha 2014/15 Toleo La Bajeti Ya Wananchi

Imechapishwa na Policy Forum

Kijitabu cha Bajeti ya Serikali toleo la mwananchi kinatolewa kuboresha upatikanaji wa taarifa za kibajeti kwa lengo la kuongeza uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa fedha za umma. Kinaelezea bajeti ya Serikali kwa lugha rahisi, ikitoa dondoo za mambo muhimu kwenye bajeti na kuifanya kuwa rahisi kwa mtu wa kawaida kuielewa. Sera na mipango iliyomo katika bajeti ya Serikali huathiri maisha ya wananchi kwa namna tofaut itofauti, hivyo ni muhimu kwao kuitafakari kikamilifu maana yake.

Muswada wa Bajeti, 2014

Imechapishwa na Policy Forum

Muswada huu unapendekeza kutungwa kwa sheria ya bajeti kwa lengo la kuweka mfumo wa kisheria utakaosimamia mchakato wa bajeti ya serikali kuanzia uandaaji, uidhinishaji, utekelezaji, ufuatiliaji, tathmini na utoaji taarifa.

Subscribe to Resources