Skip to main content

Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini: Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGDG)

Imechapishwa na Policy Forum

Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya tathmini ya mwaka na ufuatiliaji wa maendeleo ya utekelezaji wa shughuli zinazogharamiwa na Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGDG) kama zinavyotekelezwa mara kwa mara na Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Uhusiano huu unatokana na ukweli kwamba ufuatiliaji unaopaswa kufanywa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa unagusa kwa kiwango kikubwa masuala yaleyale au maeneo muhimu ambayo hufanyiwa tathmini wakati wa upimaji wa mwaka.

Mwongozo wa Utekelezaji na Uendeshaji: Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGDG)

Imechapishwa na Policy Forum

Serikali imedhamiria kutekeleza Sera ya Ugatuaji wa Madaraka ambapo moja ya mambo ya msingi katika Sera hiyo ni ugatuaji wa masuala ya fedha kupitia eneo hili. MSM zinawezeshwa kifedha kufanya maamuzi yanayohusu maeneo yao ili kukidhi mahitaji yaliyobainishwa kwenye maeneo yao na kutekeleza programu na shughuli zinazotokana na mahitaji hayo. Kwa hiyo, ugatuaji wa masuala ya fedha, una maana kwamba MSM zinawekewa masharti ya kifedha kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yao kupitia mapato ya ndani na mapato kutoka Serikali Kuu kwa uwazi na usawa.

Tamko La Umoja Wa Wadau Wa Haki Ya Kodi Tanzania (Ttjc): Ukusanyaji Wa Mapato Yatokanayo Na Rasilimali Za Ndani, Matumizi, Changamoto Na Mapendekezo

Imechapishwa na Policy Forum

TAMKO LA UMOJA WA WADAU WA HAKI YA KODI TANZANIA (TTJC)

UKUSANYAJI WA MAPATO YATOKANAYO NA RASILIMALI ZA NDANI, MATUMIZI, CHANGAMOTO NA MAPENDEKEZO

Serikali inalo jukumu kubwa la kuwapatia wananchi huduma bora za umma. Ili Serikali iweze kutimiza wajibu wake kwa umma inahitaji rasilimali mbalimbali, zikiwemo fedha. Kushindwa kwa serikali kukusanya mapato ya kutosha kunadhoofisha uwezo wake wa kutoa huduma bora kwa Watanzania.

Hotuba Ya Waziri Wa Nchi Ofisi Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa (Or-Tamisemi) Mhe. Selemani Jafo (Mb) Wakati Wa Uzinduzi Wa Miongozo Ya Mfumo Wa Utoaji Wa Ruzuku Ya Maendeleo Ya Serikali Za Mitaa (Lgdg) Mjini Dodoma, 28 Oktoba 2017

Imechapishwa na Policy Forum

HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (OR-TAMISEMI) MHE. SELEMANI JAFO (MB) WAKATI WA UZINDUZI WA MIONGOZO YA MFUMO WA UTOAJI WA RUZUKU YA MAENDELEO YA SERIKALI ZA MITAA (LGDG) MJINI DODOMA, 28 OKTOBA 2017

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Dodoma,

Wenyeviti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Bahi,

Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Dodoma,

Kikundi Kazi Cha Policy Forum Na Or-Tamisemi Wajadiliana Jinsi Ya Kuboresha Utendaji Katika Ngazi Za Serikali Za Mitaa Nchini

Imechapishwa na Policy Forum

Halmashauri nchini zimeshauriwa kubuni vyanzo vipya vya mapato ili ziweze kupata mapato ambayo yatasaidia katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo katika ngazi ya serikali za mitaa. Hayo yamesemwa Oktoba 27, 2017 mjini Dodoma na wawakilishi wa idara mbalimbali za Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) wakati wa mkutano uliojumuisha wanachama wa Policy Forum (PF) na maafisa wa OR-TAMISEMI.

Ripoti Fupi Ya Uchambuzi Wa Bajeti Ya Wizara Ya Nishati Na Madini Kwa Mwaka 2017/2018

Imechapishwa na Policy Forum

Sekta ya nishati inakabiliwa na changamoto mbalimbali hapa nchini ikiwemo: upungufu wa fedha za kutosha, ushiriki na uwekezaji mdogo wa sekta binafsi katika miradi mikubwa ya nishati; utegemezi mkubwa sana kwa tungamotaka kama chanzo cha nishati; gharama kubwa za tozo za uunganishaji na usambazaji wa umeme; upungufu wa wataalam na tafiti; uwepo na matumizi ya teknolojia miundombinu duni; na uwekezaji mdogo katika nishati jadidifu. Soma zaidi...

Uchambuzi Wa Utekelezaji Wa Mapato Na Matumizi Ya Mwaka 2016/2017 Na Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Kwa Mwaka 2017/2018

Imechapishwa na Policy Forum

Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni sekta muhimu sana kwa uchumi na maendeleo ya nchi na Watanzania
kiujumla. Sekta hizi zimeendelea kuwa chanzo kikubwa cha kipato kwa zaidi ya asilimia 65 ya
Watanzania na nguzo muhimu katika kuhakikisha usalama wa chakula, na zinachangia pato la taifa
kwa zaidi ya asilimia 29 na kwa mauzo ya nje zinachangia kwa zaidi ya asilimia 24.

Viwango vya Utawala Bora na Usimamizi wa Rasilimali Asilia (RGI) hutathmini jinsi nchi zenye utajiri wa rasilimali za Mafuta, Gesi na Madini zinavyojisimamia

Imechapishwa na Policy Forum

Sekta ya Mafuta na Gesi asilia ina alama 53 kati ya alama 100 za RGI 2017. Tofauti na sekta ya madini ambayo ni kongwe, Tanzania bado haijaanza uzalishaji mkubwa wa gesi baada ya ugunduzi wa gesi nyingi katika kina kirefucha bahari ya Hindi  ambayo hivi sasa inakadiriwa kuwa futi za ujazo trilioni 57. Hali ya kuridhisha ya Tanzania katika uwezekano wa kupata thamani ya rasilimali, kipengele kinachopima ubora wa utawala katika utoaji wa leseni, mfumo wa kodi, athari kwa jamii na ushiriki wa Serikali, hutegemea sana utaratibu wa kisheria wenye masharti mahimu kuhusu utawala na uwazi.

Mapitio ya " Suala la Dola Bilioni Moja": Tanzania Inaendelea Kupoteza Kiasi Gani cha Fedha za Kodi?

Imechapishwa na Policy Forum

Serikali inalo jukumu kubwa la kuwahakikishia na kuwapatia watu wake huduma na bidhaa za umma. Hizi ni pamoja na afya, elimu, maji, miundombinu, ulinzi na usalama na kadhalika. Huduma na bidhaa hizi ni muhimu sana ili wananchi waweze kustawi na kuondokana na matatizo kama vile umaskini, ujinga na maradhi.Huduma na bidhaa za umma hugharimu rasilimali nyingi zikiwemo fedha. Fedha hizi ni za kutoka ndani na nje ya nchi. Fedha za ndani ni pamoja na mapato ya kikodi na yasiyo ya kikodi.

Subscribe to Resources