Skip to main content

Utozaji Kodi kwa Miji Inayokuwa Tanzania: Ukusanyaji wa Kodi ya Majengo kati ya Serikali Kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa

Imechapishwa na Policy Forum

Ufanisi wa mfumo wowote ule wa kukusanya kodi za majengo unahitaji ushirikiano imara kati ya Mamlaka ya Ukusanyaji wa Kodi na Halmashauri za Miji/Majiji. Aidha, ni budi kuwepo na mgawanyo ulio wazi na bayana wa majukumu na madaraka ya mamlaka hizo. Katika miaka kumi iliyopita mfumo wa kukusanya kodi ya majengo katika Tanzania umekuwa ukibadilika mara kwa mara kati ya mfumo wa kugatua madaraka kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mfumo wa kukusanya kodi hiyo moja kwa moja kwa kutumia Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi ya Serikaali Kuu.

Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari: Maoni Ya Kikundi Kazi Cha Bajeti Cha Policy Forum Kuhusu Bajeti Ya Taifa 2018/2019

Imechapishwa na Policy Forum

Dodoma, Julai 17 2018

Tarehe 14 mwezi wa Juni 2018 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Philip Mpango aliwasilisha Bungeni Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2018/19 kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa na Bunge ili kuruhusu utekelezaji wake ifikapo Julai Mosi 2018. Hotuba hii ya Waziri ilitanguliwa na mawasilisho ya bajeti za Wizara mbalimbali pamoja na mijadala.

Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP II): Ni kwa Jinsi Gani Tutaboresha Utekelezaji Katika Mamlaka ya Serikali za Mtaa?

Imechapishwa na Policy Forum

Mwanzoni mwa mwaka 2016, Serikali ilizindua FYDP II, kwa lengo la kurekebisha mapungufu ya FYDP I na kutoa mpango makini wakati Tanzania inapoanza kuelekea katika maendeleo ya viwanda katika miaka mitano ijayo (2016 – 2021).

Katika kufanya marejeo ya FYDP I, serikali ilitambua kuwa mpango wa awali ulishindwa kufanikisha malengo yake mengi. Wakati Serikali imedhamiria kuwa ukuzaji wa viwanda ni kipaumbele katika miaka mitano ijayo, mapungufu ndani ya mpango unaweza kufanya nchi ishindwe kwa mara nyingine tena kama masuala yaliyojitokeza hayajafanyiwa kazi vya kutosha.

Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini: Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGDG)

Imechapishwa na Policy Forum

Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya tathmini ya mwaka na ufuatiliaji wa maendeleo ya utekelezaji wa shughuli zinazogharamiwa na Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGDG) kama zinavyotekelezwa mara kwa mara na Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Uhusiano huu unatokana na ukweli kwamba ufuatiliaji unaopaswa kufanywa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa unagusa kwa kiwango kikubwa masuala yaleyale au maeneo muhimu ambayo hufanyiwa tathmini wakati wa upimaji wa mwaka.

Mwongozo wa Utekelezaji na Uendeshaji: Mfumo wa Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGDG)

Imechapishwa na Policy Forum

Serikali imedhamiria kutekeleza Sera ya Ugatuaji wa Madaraka ambapo moja ya mambo ya msingi katika Sera hiyo ni ugatuaji wa masuala ya fedha kupitia eneo hili. MSM zinawezeshwa kifedha kufanya maamuzi yanayohusu maeneo yao ili kukidhi mahitaji yaliyobainishwa kwenye maeneo yao na kutekeleza programu na shughuli zinazotokana na mahitaji hayo. Kwa hiyo, ugatuaji wa masuala ya fedha, una maana kwamba MSM zinawekewa masharti ya kifedha kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yao kupitia mapato ya ndani na mapato kutoka Serikali Kuu kwa uwazi na usawa.

Tamko La Umoja Wa Wadau Wa Haki Ya Kodi Tanzania (Ttjc): Ukusanyaji Wa Mapato Yatokanayo Na Rasilimali Za Ndani, Matumizi, Changamoto Na Mapendekezo

Imechapishwa na Policy Forum

TAMKO LA UMOJA WA WADAU WA HAKI YA KODI TANZANIA (TTJC)

UKUSANYAJI WA MAPATO YATOKANAYO NA RASILIMALI ZA NDANI, MATUMIZI, CHANGAMOTO NA MAPENDEKEZO

Serikali inalo jukumu kubwa la kuwapatia wananchi huduma bora za umma. Ili Serikali iweze kutimiza wajibu wake kwa umma inahitaji rasilimali mbalimbali, zikiwemo fedha. Kushindwa kwa serikali kukusanya mapato ya kutosha kunadhoofisha uwezo wake wa kutoa huduma bora kwa Watanzania.

Hotuba Ya Waziri Wa Nchi Ofisi Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa (Or-Tamisemi) Mhe. Selemani Jafo (Mb) Wakati Wa Uzinduzi Wa Miongozo Ya Mfumo Wa Utoaji Wa Ruzuku Ya Maendeleo Ya Serikali Za Mitaa (Lgdg) Mjini Dodoma, 28 Oktoba 2017

Imechapishwa na Policy Forum

HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (OR-TAMISEMI) MHE. SELEMANI JAFO (MB) WAKATI WA UZINDUZI WA MIONGOZO YA MFUMO WA UTOAJI WA RUZUKU YA MAENDELEO YA SERIKALI ZA MITAA (LGDG) MJINI DODOMA, 28 OKTOBA 2017

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Dodoma,

Wenyeviti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Bahi,

Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Dodoma,

Kikundi Kazi Cha Policy Forum Na Or-Tamisemi Wajadiliana Jinsi Ya Kuboresha Utendaji Katika Ngazi Za Serikali Za Mitaa Nchini

Imechapishwa na Policy Forum

Halmashauri nchini zimeshauriwa kubuni vyanzo vipya vya mapato ili ziweze kupata mapato ambayo yatasaidia katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo katika ngazi ya serikali za mitaa. Hayo yamesemwa Oktoba 27, 2017 mjini Dodoma na wawakilishi wa idara mbalimbali za Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) wakati wa mkutano uliojumuisha wanachama wa Policy Forum (PF) na maafisa wa OR-TAMISEMI.

Subscribe to Resources