Skip to main content

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania - Mwongozo wa Jamii za Kiraia

Imechapishwa na Policy Forum

Bajeti kwa kawaida imekuwa ikichukuliwa kuwa ni kazi ya wataalamu, wachumi na wahasibu tu. Lakini uamuzi wa Serikali wa namna gani ya kukusanya mapato huwaathiri wananchi wote. Kiwango cha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kodi nyingine huathiri bei za vitu vinavyotumiwa katika kaya. Uamuzi wa matumizi ya serikali ndio huweka wazi iwapo viwango vya mishahara ya walimuna iwapo kutakuwa na dawa na vifaa vya kutosha katika zahanati au la.

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania - Mwongozo wa Jamii za Kiraia

Imechapishwa na Policy Forum

Bajeti kwa kawaida imekuwa ikichukuliwa kuwa ni kazi ya wataalamu, wachumi na wahasibu tu. Lakini uamuzi wa Serikali wa namna gani ya kukusanya mapato huwaathiri wananchi wote. Kiwango cha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kodi nyingine huathiri bei za vitu vinavyotumiwa katika kaya. Uamuzi wa matumizi ya serikali ndio huweka wazi iwapo viwango vya mishahara ya walimuna iwapo kutakuwa na dawa na vifaa vya kutosha katika zahanati au la.

Tamko La Asasi Za Kiraia Juu Ya Mafanikio Na Madhara Kwa Tanzania Kuendelea Kutumia Ushauri Wa IMF

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi wajumbe wa Asasi za kiraia za ki-Tanzania tuliokutana leo ukumbi wa Dar es Salaam International Conference Centre, tarehe 10 Machi 2009 kwa uratibu wa mtandao wa Policy Forum, Human Development Trust na Tanzania AIDs Forum, baada ya kujadili na kutafakari kwa kina taarifa za ''mafanikio'' ya utekelezaji mipango ya IMF na sera za Tanzania ki-uchumi kwa miaka ya 2000 hadi 2008 tumebaini yafuatayo:-

1. Ni kweli takwimu zinaonesha kukua kwa uchumi kwa wastani wa zaidi ya asilimia 7% kwa kipindi tajwa,

Nioneshe Pesa Ziliko

Imechapishwa na Policy Forum

Katika miezi ya hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko la madai ya uwajibikaji kutoka kwa Wabunge ambayo yamebadilisha muonekano wa Bunge na yamepelekea kujiuzuru kwa mawaziri kadhaa, ikiwa ni pamoja na Waziri Mkuu. Mswada wa Sheria ya Ukaguzi imepelekwa Bungeni chini ya hati ya dharura na itajadiliwa katika kikao kijacho cha Bajeti mwaka huu. Mswada huu unalenga kuiongezea Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAO) uhuru mkubwa wa kutoingiliwa na Dola katika utendaji wake wa kumsaidia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Ufafanuzi Wa Mikataba Ya Madini Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Zipo nyaraka nyingi zinazoonesha kuwa Tanzania imejaliwa madini mbalimbali yakiwamo almasi, dhahabu, na madini ya vito yasiyopatikana mahali pengine popote duniani, Tanzanite.

Hivi karibuni, sekta ya madini iliwekwa kwenye kipaumbele na Serikali ya Tanzania kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuchangia katika ukuaji wa haraka wa uchumi wa nchi.

Ripoti ya Bomani - Taarifa fupi ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali kuhusu Usimamizi wa Sekta ya Madini

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum tunayo furaha kuchapisha kitabu hiki ambacho kinatokana na ‘Taarifa ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali Kuhusu Usimamizi wa Sekta ya Madini’ Juzuu Namba 2.

Shukrani kwa Reginald Martin wa LHRC kwa ushirikiano wake wa hali na mali ikiwa ni pamoja na kutumia muda wake kuhakikisha anaihariri Taarifa hii fupi. Bila kumsahau mchora katuni wetu Nathan Mpangala.

Msimamo wa Wanachama wa Policy Forum kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo

Imechapishwa na Policy Forum

Wanachama wa Policy Forum, tukiwa ni sehemu ya jumuiya za kiraia na sehemu ya wapiga kura wa wabunge wetu tumechukua jukumu katika jukwaa hili leo kutoa tahadhari kwa wabunge wetu kuhusu athari za kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo ya jimbo. Hii ni sehemu muhimu ya wajibu wetu kama raia waaminifu, wenye nia njema ya kuchangia mawazo bora yatakayotuletea maendeleo endelevu nchini kwetu. Bila mjadala mpana na mawazo chanya yaliyochambua maswala kwa undani kama msingi wa maamuzi, nchi itafanya maamuzi dhaifu yasiosimama kwenye misingi ya hoja na ukweli wa mambo.

KIFO CHA MWANAMKE MJAMZITO MWANANYAMALA HOSPITALI - FEMACT

Imechapishwa na Policy Forum

Tumepokea na kufuatilia mkanganyiko wa sababu za kifo cha mama mjamzito (Tedy Dimoso) na kichanga wake wakati wa kujifungua kwa masikitiko makubwa sana. Kwa mujibu wa barua kutoka kwa msimamizi wa mirathi kifo hiki kilitokea tarehe 01/06/2008 katika hospitali ya Mwananyamala. Barua hiyo ya tarehe 06/06/2008 kwenda kwa Waziri wa Afya inatoa maelezo kwa kina jinsi kifo hicho kinavyoweza kuwa kimetokea kwa uzembe.

Utawala Wa Kidemokrasia Katika Jamii: Ushiriki Wa Wananchi Katika Serikali Za Mitaa (Vitongoji, Vijiji Na Mitaa)

Imechapishwa na Policy Forum

Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum (LGWG) kimechapisha tafsiri rahisi ya kanuni za utawala kijijini. Kitabu hicho kinachoitwa 'UTAWALA WA KIDEMOKRASIA KATIKA JAMII: USHIRIKI WA WANANCHI KATIKA SERIKALI ZA MITAA (VITONGOJI, VIJIJI NA MITAA)', kinalenga kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mipango ya maendeleo katika vijiji na mitaa. Kama kawaida ya Policy Forum, kitabu hiki kiko kwa lugha rahisi na katuni ili kumpa hamu msomaji na kuongeza uelewa zaidi wa ujumbe kwa kile kilichokusudiwa kufika kwa mwananchi wa kawaida.

Subscribe to Resources