Skip to main content

Ufafanuzi Wa Mikataba Ya Madini Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Zipo nyaraka nyingi zinazoonesha kuwa Tanzania imejaliwa madini mbalimbali yakiwamo almasi, dhahabu, na madini ya vito yasiyopatikana mahali pengine popote duniani, Tanzanite.

Hivi karibuni, sekta ya madini iliwekwa kwenye kipaumbele na Serikali ya Tanzania kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuchangia katika ukuaji wa haraka wa uchumi wa nchi.

Ripoti ya Bomani - Taarifa fupi ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali kuhusu Usimamizi wa Sekta ya Madini

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum tunayo furaha kuchapisha kitabu hiki ambacho kinatokana na ‘Taarifa ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali Kuhusu Usimamizi wa Sekta ya Madini’ Juzuu Namba 2.

Shukrani kwa Reginald Martin wa LHRC kwa ushirikiano wake wa hali na mali ikiwa ni pamoja na kutumia muda wake kuhakikisha anaihariri Taarifa hii fupi. Bila kumsahau mchora katuni wetu Nathan Mpangala.

Msimamo wa Wanachama wa Policy Forum kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo

Imechapishwa na Policy Forum

Wanachama wa Policy Forum, tukiwa ni sehemu ya jumuiya za kiraia na sehemu ya wapiga kura wa wabunge wetu tumechukua jukumu katika jukwaa hili leo kutoa tahadhari kwa wabunge wetu kuhusu athari za kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo ya jimbo. Hii ni sehemu muhimu ya wajibu wetu kama raia waaminifu, wenye nia njema ya kuchangia mawazo bora yatakayotuletea maendeleo endelevu nchini kwetu. Bila mjadala mpana na mawazo chanya yaliyochambua maswala kwa undani kama msingi wa maamuzi, nchi itafanya maamuzi dhaifu yasiosimama kwenye misingi ya hoja na ukweli wa mambo.

KIFO CHA MWANAMKE MJAMZITO MWANANYAMALA HOSPITALI - FEMACT

Imechapishwa na Policy Forum

Tumepokea na kufuatilia mkanganyiko wa sababu za kifo cha mama mjamzito (Tedy Dimoso) na kichanga wake wakati wa kujifungua kwa masikitiko makubwa sana. Kwa mujibu wa barua kutoka kwa msimamizi wa mirathi kifo hiki kilitokea tarehe 01/06/2008 katika hospitali ya Mwananyamala. Barua hiyo ya tarehe 06/06/2008 kwenda kwa Waziri wa Afya inatoa maelezo kwa kina jinsi kifo hicho kinavyoweza kuwa kimetokea kwa uzembe.

Utawala Wa Kidemokrasia Katika Jamii: Ushiriki Wa Wananchi Katika Serikali Za Mitaa (Vitongoji, Vijiji Na Mitaa)

Imechapishwa na Policy Forum

Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum (LGWG) kimechapisha tafsiri rahisi ya kanuni za utawala kijijini. Kitabu hicho kinachoitwa 'UTAWALA WA KIDEMOKRASIA KATIKA JAMII: USHIRIKI WA WANANCHI KATIKA SERIKALI ZA MITAA (VITONGOJI, VIJIJI NA MITAA)', kinalenga kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mipango ya maendeleo katika vijiji na mitaa. Kama kawaida ya Policy Forum, kitabu hiki kiko kwa lugha rahisi na katuni ili kumpa hamu msomaji na kuongeza uelewa zaidi wa ujumbe kwa kile kilichokusudiwa kufika kwa mwananchi wa kawaida.

Warsha kuhusu Mpango wa Kurekebisha Serikali za Mitaa - Ripoti ya Awali

Imechapishwa na Policy Forum

Tarehe 26 na 27 Novemba 2007, Kikundi-kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum ikisaidiwa na Leadership Forum, kiliandaa warsha kuhusu mwelekeo wa Programu ya Kurekebisha Serikali za Mitaa kilichofanyika mji wa Kibaha. Dhumuni kuu lilikuwa kuwapa fursa maafisa wa TAMISEMI kutoa taarifa kwa wadau kutoka asasi mbalimbali kuhusu maendeleo ya programu hiyo. Vilevile, ilikuwa fursa kwa asasi kuwapa TAMISEMI maoni kuhusu programu inayofuata (2008 – 2013).

Prevention and Combating of Corruption Act 2007

Imechapishwa na Policy Forum

Together with the Prevention and Combating of Corruption Bureau  (PCCB), Policy Forum Prevention this year published the popular version of the Prevention and Combating of Corruption Act 2007 (article 11) in Swahili entitled: IFAHAMU SHERIA MPYA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA NCHINI NAMBA 11 YA MWAKA 2007.

The booklet is in pdf format click here to see the cover page and here to see the booklet

Jukwaa issue 3

Imechapishwa na Policy Forum

This issue is on the topic of decentralisation. Where is Management of Public Money Most Accountable - at Central or Local level?. bofya hapa kuisoma

Subscribe to Resources