Warsha kuhusu Mpango wa Kurekebisha Serikali za Mitaa - Ripoti ya Awali
Tarehe 26 na 27 Novemba 2007, Kikundi-kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum ikisaidiwa na Leadership Forum, kiliandaa warsha kuhusu mwelekeo wa Programu ya Kurekebisha Serikali za Mitaa kilichofanyika mji wa Kibaha. Dhumuni kuu lilikuwa kuwapa fursa maafisa wa TAMISEMI kutoa taarifa kwa wadau kutoka asasi mbalimbali kuhusu maendeleo ya programu hiyo. Vilevile, ilikuwa fursa kwa asasi kuwapa TAMISEMI maoni kuhusu programu inayofuata (2008 – 2013).