Skip to main content

Tangazo la Policy Forum la Uwazi na Uziduaji katika Sekta ya Madini

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum imetoa tangazo juu ya Sekta ya nishati na madini Tanzania ambalo kwa sasa linarushwa hewani katika vituo viwili vya Televisheni ambavyo ni ITV na Star TV. Lengo la tangazo ni kuwafanya raia wa kawaida wa Tanzania kuuliza viongozi wao juu ya rasilimali ya madini yao ambayo inapaswa kutumiwa kwa manufaa ya watanzania na si vinginevyo. Ona tangazo chini 

Tamko La Ngurdoto La Kamati Ya Viongozi Wa Dini Na Asasi Za Kiraia Oktoba 20, 2011

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi, Kamati ya Viongozi wa Dini kwa Masuala ya Kijamii, Uchumi, Haki na Uhifadhi wa Mazingira na Maumbile na wanachama wa Policy Forum, tuliokutana katika Mkutano Mbadala wa masuala ya Madini mjini Arusha tarehe 20 Oktoba 2011, tumejadili kwa kina madhara yatokanayo na shughuli za uchimbaji wa madini katika jamii zionazoishi karibu na migodi ya madini na kwa mazingira, na tunaiomba serikali na Bunge kuhakikisha kuwa zinatekeleza kwa dhati majukumu

Policy Forum Kuzindua Mapitio Ya Utawala Wa Tanzania 2008/09

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum kwa kushirikiana na Tanzania Development Research Group (TADREG), imechapisha mapitio ya utawala wa Tanzania wa pili ambao unachunguza nyaraka za serikali rasmi, takwimu, taarifa kutoka mashirika ya misaada, machapisho kutoka taasisi za elimu, mashirika ya kiraia na makala kutoka vyombo vya habari kwa madhumuni ya taarifa juu ya mwenendo wa utawala katika Tanzania.

Mkakati Wa Pamoja Wa Uratibu Na Matumizi Bora Ya Misaada

Imechapishwa na Policy Forum

Mchakato wa kuhalalisha mahusiano baina ya Serikali, wahisani, wafadhili na Asasi zizo za kiserikali AZAKI umekuwa na changamoto nyingi. Kumekew na juhudi nyingi ambazo zimekuwa zikitoa tumaini kwa AZAKI kwamba mahusiano rasmi na wadau wengine wa maendeleo ni jambo ambalo linawezekana kuwa rasmi na endelevu.

Subscribe to Resources