Skip to main content

Warsha ya Asasi za Kiraia Juu ya Viwango Vipya vya Mpango wa Uwazi wa Tasnia ya Uziduaji (EITI)

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum kwa kushirikiana na Mpango wa Uhamasishaji Uwazi katika Mapato ya Madini, Gesi asilia na Mafuta Tanzania ( TEITI ) pamoja na Hakimadini wameandaa warsha ( 2-3 Aprili 2014) Arusha kwa lengo la kuwawezesha wawakilishi wa asasi za kiraia za kaskazini mwa Tanzania zinazofanya kazi katika masuala ya uziduaji kuongeza uelewa wao wa viwango vipya vya  Mpango wa Uhamasishaji Uwazi katika Mapato ya Madini au Mpango wa Uwazi katika Tasnia ya Uziduaji (EITI) ili kuongeza uwezo wao wa kuiwajibisha serikali yao.

Rasimu ya Pili ya KATIBA Inasemaje? Chapisho la Lugha Nyepesi

Imechapishwa na Policy Forum

Tanzania ipo katika mchakato wa Katiba tangu mwanzoni mwa mwaka 2011. Hatua kadhaa zimeshapitiwa katika mchakato huu muhimu kwa Taifa letu kama ifuatavyo; Kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya
mwaka 2011, kuundwa kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa mujibu wa sheria, Tume kuanza kazi kwa kukusanya maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya, Tume kutoa Rasimu ya kwanza ya Katiba na hatimaye Rasimu ya pili
ya Katiba.

Ushindani wa Kodi Afrika ya Mashariki:Mbio za kuelekea chini? Motisha ya Kodi na Upotevu wa Mapato Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Serikali ya Tanzania inatoa wigo mpana wa motisha wa kodi kwa wafanya biashara ili kuvutia viwango vikubwa zaidi vya uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (FDIs) nchini.

Utoaji wa motisha ya kodi Tanzania, tunaweza kusema ni sehemu ya ushindani wa kodi miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika ya Mashariki (EAC). Kufuatia uundaji wa EAC mwaka 1999, Kenya, Tanzania, na Uganda walianzisha umoja wa forodha (eneo ambalo halina ushuru wa forodha na lenye kiwango cha tozo ya bidhaa zinazotoka nje ya nchi kinachofanana) mwaka 2005, na Rwanda na Burundi wakajiunga mwaka 2009.

Mkutano Wa Uwazi Katika Usimamizi Wa Fedha Wavuta Hadhira Ya Kimataifa

Imechapishwa na Policy Forum

Mtandao wa Uwazi Katika usimamizi wa Fedha “The Financial Transparency Coalition (FTC)’ na asasi mwenyeji ya Policy Forum, wameandaa mkutano mahiri katika uwazi wa usimamizi wa fedha. Mada kuu ya mkutano huo wa siku mbili unaofanyika Jumanne  na Jumatano wiki hii katika Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam, ni “Kuleta Uwazi: Namna ya Kujenga Uwazi wa Matumizi ya Fedha Duniani kwa Ajili ya Maendeleo”.

Subscribe to PF-related