Skip to main content

Tamisemi Kushirikiana na AZAKI kuandaa Mwongozo wa Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu Wenye Ulemavu

Imechapishwa na Policy Forum

Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017-2020/21), pamoja na malengo mengine, unakusudia kuweka mazingira wezeshi kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kimaendeleo kama vile uvuvi, kilimo, ufugaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.

Miongoni mwa mikakati iliyowekwa na Serikali ya kutimiza lengo la kusaidia makundi hayo ni utoaji wa mikopo isiyo na riba.

Kanuni za Utoaji wa Mikopo na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu za Mwaka 2019

Imechapishwa na Policy Forum

Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017-2020/21), pamoja na malengo mengine, unakusudia kuweka mazingira wezeshi kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kiuchumi kama vile kilimo, ufugaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.

Miongoni mwa mikakati ya kutimiza lengo hilo iliyoainishwa katika Mpango huo ni utoaji wa mikopo yenye gharama na masharti nafuu kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Zijue Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa: Ngazi ya Vijiji, Mitaa na Vitongoji, 2019

Imechapishwa na Policy Forum

 Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 8(1) (a); wananchi ndio chimbuko la mamlaka ya utawala wa nchi na kwamba Serikali itapata mamlaka kutoka kwao. Uchaguzi ndio namna pekee ya wananchi kukasimisha mamlaka yao kwa viongozi. Ni Haki ya kila raia kushiriki katika michakato ya Uchaguzi ikiwemo kupiga au kupigiwa kura kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi ili kupata viongozi.

Sekta ya Kilimo na Mifugo Yatajwa Kama Chachu ya Kufikia Uchumi wa Viwanda

Imechapishwa na Policy Forum

Wanachama wa mtandao wa Policy Forum wanaounda kikundi kazi cha bajeti (BWG) wameishauri serikali kuboresha sekta ya kilimo na ufugaji ili nchi iweze kufikia azimio lake la kuhakikisha inafikia uchumi wa kati wenye kuchagizwa na viwanda. Hayo yamesemwa tarehe 4 Mei 2019 Jijini Dodoma ambapo wanachama hao walikutana na wabunge wa kamati ya bajeti na mtandao wa kupambana na rushwa wa afrika tawi la Tanzania (APNAC-TANZANIA).

Uswisi kushirikiana na Tanzania kuimarisha uwajibikaji

Imechapishwa na Policy Forum

Ubalozi wa Uswisi hapa nchini kupitia Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi SDC umezindua awamu ya tatu ya programu ya uwajibikaji wa kijamii (Social Accountability Programme - SAP) ambayo inachangia kuziwezesha asasi za kiraia (AZAKI) zinazofanya kazi ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania.

Tamko La Policy Forum Na Wadau Wengine Juu Ya; Mapendekezo Ya Kuboresha Sheria Ya Takwimu

Imechapishwa na Policy Forum

Kufuatia kupitishwa kwa sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2018,  Sisi wadau kutoka Asasi za Kiraia na watafutaji, watumiaji na wasambazaji wa taarifa za takwimu tumekutana kufanya uchambuzi wa kina wa sheria hii;

Pamoja na kutambua umuhimu wa sheria hii ambayo imelenga kuzuia usambazaji/ uchapishaji wa taarifa za kitakwimu zinazoweza kupotosha umma;

Mkurugenzi wa TAKUKURU Afurahishwa na Kampeni ya Kudhibiti Upotevu wa Fedha za Umma

Imechapishwa na Policy Forum

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema imefurahishwa na kampeni ya Policy Forum iitwayo Stop the Bleeding ambayo inahusu udhibiti wa upotevu wa fedha za Umma kupitia njia haramu zikiwemo utakatishaji wa fedha na ukwepaji kodi. Hayo yamesemwa Novemba 11, 2018 Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Diwani Athumani alipokuwa akiongea na Wabunge wa Bunge Tanzania Wanaopamba na Rushwa (APNAC).

Mikataba ya utozaji kodi mara mbili (DTAs) na hatma yake kwa nchi

Imechapishwa na Policy Forum

Mwaka 2018 Policy Forum (PF) mtandao wa asasi zaidi ya 70 zilizosajiliwa Tanzania ilichapisha utafiti unaohusu mikataba ya utozaji kodi mara mbili (Double Taxation Agreements - DTAs) kati ya Tanzania na Afrika Kusini na Tanzania na India. Makala hii ni tafsiri ya muhtasari wa utafiti huo ambao ulitumika kwenye kikao cha pamoja na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao wapo kwenye Mtandao wa Kupambana na Rushwa (APNAC) mnamo Novemba 8, 2018 Jijini Dodoma.

Subscribe to PF-related