Skip to main content

Social Accountability

Midahalo ya Raia Makini Yafichua Mianya ya Uwajibikaji

Imechapishwa na Policy Forum

Midahalo ya umma iliyofanyika chini ya mradi wa Raia Makini imebainisha changamoto kubwa zinazowakabili wananchi katika upangaji na utekelezaji wa bajeti za serikali za mitaa, huku ikiongeza utayari wa wananchi kushirikiana na viongozi katika usimamizi wa rasilimali za umma. Midahalo hiyo imeonesha wazi kuwa wananchi wanapopewa taarifa sahihi na nafasi salama ya kujieleza, wako tayari kuuliza maswali, kudai uwajibikaji na kuchangia kwa njia chanya maendeleo ya maeneo yao.

Wananchi Wahimizwa Kuchukua Nafasi ya Uongozi Wahimizwa Kushiriki Katika Maamuzi ya Maendeleo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika

Imechapishwa na Policy Forum

Mdahalo wa wa asubuhi chini ya mradi wa Raia Makini ulifanyika tarehe 17 Novemba 2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, mkoani Katavi. Lengo kuu lilikuwa kuangazia umuhimu wa ushiriki wa wananchi katika upangaji wa mipango na bajeti, pamoja na namna Halmashauri inavyotarajia kuwawezesha wananchi kushiriki katika mchakato wa bajeti.

Vinara wa Uwajibikaji Wajengewa Uwezo Kuhusu Mfumo Ulioboreshwa wa O&OD na Mchakato wa Bajeti katika Ngazi ya Msingi

Imechapishwa na Policy Forum

 

Vinara wa Uwajibikaji (Community Accountability Champions – CACs) kutoka wilaya za Tanganyika mkoani Katavi na Mpwapwa mkoani Dodoma wamejengewa uwezo kupitia mafunzo maalum yaliyoratibiwa chini ya mradi wa Raia Makini, unaotekelezwa na Wajibu – Institute of Public Accountability kwa kushirikiana na Policy Forum, kwa ufadhili wa pamoja kutoka Umoja wa Ulaya (EU).

Uswisi kushirikiana na Tanzania kuimarisha uwajibikaji

Imechapishwa na Policy Forum

Ubalozi wa Uswisi hapa nchini kupitia Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswisi SDC umezindua awamu ya tatu ya programu ya uwajibikaji wa kijamii (Social Accountability Programme - SAP) ambayo inachangia kuziwezesha asasi za kiraia (AZAKI) zinazofanya kazi ili kuboresha uwajibikaji nchini Tanzania.

Subscribe to SA