Skip to main content

Ushindani wa Kodi Afrika ya Mashariki:Mbio za kuelekea chini? Motisha ya Kodi na Upotevu wa Mapato Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Serikali ya Tanzania inatoa wigo mpana wa motisha wa kodi kwa wafanya biashara ili kuvutia viwango vikubwa zaidi vya uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (FDIs) nchini.

Utoaji wa motisha ya kodi Tanzania, tunaweza kusema ni sehemu ya ushindani wa kodi miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika ya Mashariki (EAC). Kufuatia uundaji wa EAC mwaka 1999, Kenya, Tanzania, na Uganda walianzisha umoja wa forodha (eneo ambalo halina ushuru wa forodha na lenye kiwango cha tozo ya bidhaa zinazotoka nje ya nchi kinachofanana) mwaka 2005, na Rwanda na Burundi wakajiunga mwaka 2009.

Policy Forum Kushiriki katika semina ya asubuhi ya ukwepaji haramu wa mitaji katika nchi maskini iliyofanyika sweden

Imechapishwa na Policy Forum

Moses Kulaba, Mwakilishi wa kikundi kazi cha bajeti akiwa anatoa mada Stockholm tarehe 23 Septemba                                                       

Tarehe 23 Septemba kikundi kazi cha Bajeti(BWG) cha Policy Forum  kilialikwa na Forum Syd na Svenska Institutet kutoa neno katika semina ya asubuhi iliyohusu ukwepaji haramu wa mitaji katika nchi maskini, jinsi gani inaathiri maendeleo, na jinsi gani inaweza kusimamishwa.               

Mada ilitoka katikati ripoti mpya ambayo Kikundi kazi cha bajeti cha Policy Forum kilikuwa mwandishi mwenza.

Subscribe to Tax