Jukwaa issue 3
This issue is on the topic of decentralisation. Where is Management of Public Money Most Accountable - at Central or Local level?. bofya hapa kuisoma
This issue is on the topic of decentralisation. Where is Management of Public Money Most Accountable - at Central or Local level?. bofya hapa kuisoma
Sakale Development Foundation (SADEF) inafanya kazi kuwasaidia Watanzania, haswa wale walio vijijini, kukabiliana na changamoto za kiuchumi, kijamii na kisiasa kupitia utafiti, mafunzo na ushauri.
Rukwa Association of NGOs (RANGO) ni shirika lisilo la kiserikali la Mkoa kwa mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyosajiliwa katika mkoa wa Rukwa. Iliandikishwa mnamo Agosti 1992 na lina wanachama 150.
Mudugu women and Community Development ( MUDUGU- WACOD) ni shirika linalofanya kazi ya kukuza / kusaidia shughuli za kuongeza kipato kwa vikundi vya wanawake na vijana. Pia ni shirika linalotoa ushauri wa kisheria (kitengo cha wasaidizi wa kisheria) elimu ya uraia na afya hasa kuhusu VVU/UKIMWI.
Community Development for All (CODEFA) ni shirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi ya kuboresha usawa na ustawi wa uchumi endelevu wa jamii za Tanzania Bara. CODEFA hufanya kazi ya kuongeza uelewa katika ngazi za chini na kuwezesha jamii kuchambua kwa kina hali zao, kutambua fursa na vizuizi kwa maendeleo, na kujipanga kwa pamoja ili kujiletea maendeleo. Lengo kuu ni kuwezesha jamii zilizo pembezoni na zilizo katika mazingira magumu kushiriki kikamilifu katika kutokomeza umaskini.
Kazi zinazofanywa na CODEFA:
Tanzania Brighter Future for Community Development Organisation (TABCO) inakusudia kuona jamii ya watanzania kutoka kwenye umasikini na shida na kuanzisha mazingira bora ya kiuchumi kwa jamii.
Kazi zinazofanywa na TABCO:
Community for Sustainable Development huwezesha jamii kutetea haki za watoto ikiwa ni pamoja na msaada wa elimu kwa watoto yatima, watoto walio katika mazingira magumu zaidi, elimu ya afya ya mama, ulinzi wa watoto, vijana na haki za kimsingi za wanawake kupitia sheria na sera mbalimbali. Pia ni asasi inayojishughulisha na masuala ya usawa wa kijinsia, uhifadhi wa mazingira , utawala bora na uwajibikaji wa kijamii na stadi za maisha ya kijamii,
Union for Non Governmental Organization (UNGO) hutoa huduma katika Mkoa wa Morogoro kwa malengo ya kuboresha maisha ya watu wa Morogoro.
Tushiriki imejitolea kushiriki katika kuleta maendeleo ya jamii masikini nchini Tanzaia. Pia ni asasi inayojishughulisha na masuala ya utawala bora, maswala ya jinsia, sera ya elimu, kilimo, PET, SAM, uharibifu wa mazingira, afya, lishe, usafi , haki za binadamu, na maji safi.
Biharamulo Originating Economic Development Association (BOSEDA) ni NGO iliyosajiliwa ambayo inashirikiana kwa karibu na wadau wengine kutoa huduma zinazokidhi mahitaji kwa jamii katika sekta za Elimu, Afya, Uhifadhi wa Mazingira, Sera za kitaifa, Jinsia, Haki za Binadamu, Utawala Bora na Demokrasia pamoja na elimu ya kiuchumi kwa kutumia rasilimali zilizopo za ndani.