Skip to main content

Sekta ya Kilimo na Mifugo Yatajwa Kama Chachu ya Kufikia Uchumi wa Viwanda

Imechapishwa na Policy Forum

Wanachama wa mtandao wa Policy Forum wanaounda kikundi kazi cha bajeti (BWG) wameishauri serikali kuboresha sekta ya kilimo na ufugaji ili nchi iweze kufikia azimio lake la kuhakikisha inafikia uchumi wa kati wenye kuchagizwa na viwanda. Hayo yamesemwa tarehe 4 Mei 2019 Jijini Dodoma ambapo wanachama hao walikutana na wabunge wa kamati ya bajeti na mtandao wa kupambana na rushwa wa afrika tawi la Tanzania (APNAC-TANZANIA).

Mgawanyo wa bajeti ya Sekta ya Kilimo: Je, nini hatma ya wakulima wadogo Tanzania?

Imechapishwa na Policy Forum

Kama sekta ya kilimoTanzania itawekezwa ipasavyo ina mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini. Kwa mujibu wa taarifa ya bajeti 2011/12 iliyotolewa na Waziri mwenye dhamana ya kilimo, kwa sasa sekta hii ina ajiri asilimia 77.5 ya watanzania na kuchangia asilimia 95 ya chakula kinachotumika nchini. Sekta ya kilimo pia inaonekana kukua kwa asilimia 4.2 tangu mwaka 2010 kutoka asilimia 3.2 ya mwaka uliotangulia.

PELUM Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

PELUM ni mtandao wa kikanda wa asasi za kiraia zaidi ya 250 katika nchi 12 za Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika zinazofanya kazi katika eneo la usimamizi shirikishi wa matumizi ya ardhi. PELUM inafanya kazi kuboresha maisha ya wakulima wadogo na uendelevu wa jamii za wakulima, kwa kukuza usimamizi wa matumizi ya ardhi.

Mbozi, Ileje and Isangati Consortium (MIICO)

Imechapishwa na Policy Forum

Mbozi, Ileje and Isangati Consortium (MIICO) ni muungano wa mashirika yanayofanya kazi na wakulima wadogo katika Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania. Ni NGO iliyosajiliwa na usajili No OONGO / 0802 chini ya sheria ya NGO Na. 24 ya 2002. Malengo makuu ya MIICO ni kuwezesha wakulima masikini na walio pembezoni mwa Tanzania kuongoza maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi ili kuboresha maisha yao.

 

SNV

Imechapishwa na Policy Forum

SNV imekuwepo nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 40. Tangu mwanzoni mwa miaka ya 2000 uchumi wa Tanzania umekuw akikua katika hali ya kuridhisha. Licha ya ukuaji huu wa uchumi, bado Tanzania inakabiliwa na tatizo la umaskini. kiwango cha umaskini bado kinasimama karibu 34% licha ya ukuaji wa uchumi wa kila mwaka wa karibu 7%.

Agricultural Non-State Actor Forum (ANSAF)

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi ni shirika lisilo la kisiasa, lisilo la kiserikali lililosajiliwa chini ya Sheria ya NGO ya Tanzania ya 2002. Tunawajibika kwa wanachama wetu kama ilivyoainishwa katika Katiba yetu na Kanuni zetu za Maadili. Mtazamo wetu juu ya uwazi na usawa hutufanya kuwa mtandao unaopendwa kwenye sekta ya kilimo.

Tunafanya kazi katika maeneo yafuatayo:

Subscribe to Agriculture