Na Jansi Sinkamba
Tamko La Asasi Za Kiraia Kuhusu Viashiria Vya Uvunjifu Wa Amani Wiki Moja Kuelekea Tarehe Ya Upigaji Kura Katika Uchaguzi Mkuu Tanzania Tarehe 25.10.2015
Asasi za Tanzania tumeendelea kufuatilia mchakato wa uchaguzi mkuu 2015 tangu uandikishaji wapiga kura, uhamasishaji hadi kampeni zinazoendelea kwa umakini mkubwa. AZAKI tumefanya hivyo tukiamini kuwa uchaguzi ni sehemu kuu ya michakato ya kidemokrasia hapa nchini kama ilivyo duniani kote. Sisi asasi za kiraia Tanzania, tukiwa watetezi na wasimamizi wa demokrasia, utawala bora na haki za binadamu, hatumuungi mkono mgombea yeyote wala chama chochote cha kisiasa kinachotafuta kuingia madarakani wala hatulengi kuchukua dola.