World vision Tanzania
Tanzania imepata ukuaji mkubwa wa uchumi katika muongo mmoja uliopita. Ingawa kiwango cha umaskini nchini kimepungua, idadi kamili ya watu maskini haijapungua kwa sababu ya kiwango cha juu cha ukuaji wa idadi ya watu. Hivyo, watoto bado wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo unyanyaswaji, utapiamlo, huduma duni za afya na elimu na huduma zingine za kimsingi.