Skip to main content
Semkae Kilonzo
Mkurugenzi Mtendaji
Contact Info
Education
Digrii ya Uzamili ya Uandishi wa Habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Uingereza
Mafuzo ya habari, Dublin, Ireland
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Semkae Kilonzo alianza kazi Policy Forum mwaka 2007 kama mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Uchechemuzi anayehusika na vyombo vya habari, ikiwa ni shauku ya mtandao kuona taarifa zinazohusiana na uchambuzi wa sera zikisambazwa kwa watunga sera, asasi za kiraia na umma kwa jumla. Akiwa kama mratibu na baadaye kama Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao amekuwa akiongoza Sekretarieti  katika majukumu ya kila siku ya kiofisi. Semkae pia ni mjumbe wa Kamati  ya Uwazi wa Bajeti, Uwajibikaji na Ushirikishwaji Global Movement for Budget Transparency, Accountability and Participation (BTAP).

Semkae ana digrii ya Uzamili ya Uandishi wa Habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Uingereza na pia amepata mafunzo kuhusu vyombo vya Habari, Dublin Ireland na pia katika  Shule ya Uandishi wa Habari Tanzania (TSJ). Semkae ni mhitumu wa mafunzo ya  Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini. Semkae anapenda sana kuhamasisha ushiriki wa umma katika utengenezaji wa sera na matumizi ya rasilimali za umma yanayozingatia usawa.

Gibons Mwabukusi
Meneja- Fedha & Utawala
Contact Info
Education
Stashahada ya Uhasibu, Taasisi ya Uhasibu Tanzania
CPA

Gibons Mwabukusi alijiunga na Policy Forum mwaka 2010 kama Afisa Fedha na Utawala. Kabla ya kujiunga na PF, Gibons alifanya kazi na AZAKI mbalimbali kama Afisa Fedha na Utawala. Ana Stashada ya Uhasibu kutoka Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) na pia ana CPA.

Richard Angelo
Meneja - Tawala Serikali za Mitaa
Contact Info
Education
Shahada ya Sanaa ya Sosholojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania
Mafunzo ya  Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini.

Richard Angelo ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo alisoma Shahada ya Sanaa katika Sosholojia na kuhitimu mnamo 2006, Hapo awali alifanya kazi HakiElimu na baadaye kama mshauri katika kitengo cha habari. Alijiunga na Policy Forum mwaka 2008 kama Msaidizi wa Programu- Vyombo vya Habari, Mawasiliano na Uchechemuzi na kwa sasa ni Meneja wa Tawaka Serikali za Mitaa. Yeye pia ni mhitimu wa mafunzo ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini na pia amehudhuria pia Mafunzo ya Wakufunzi (ToT) ya SAM.

Elinami John
Meneja - Uchechemuzi & Ushirikishaji
Contact Info
Education
Shahada ya Uzamili katika Vyombo vya Habari na Mawasiliano, Chuo Kikuu cha Karlstad, Uswidi
Shahada ya Sanaa katika Mahusiano ya Umma na Matangazo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Elinami John alijiunga na Policy Forum mnamo Septemba, 2016. Hapo awali alifanya kazi kama afisa programu anayesimamia upatikanaji wa taarifa na uhuru wa vyombo vya habari katika Baraza la Habari Tanzania (MCT). Alimaliza shahada yake ya kwanza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania. Ana shahada ya Uzamili katika Vyombo vya Habari na Mawasiliano kutoka Chuo Kikuu cha Karlstad, Uswidi. Anapenda zaidi kuchunguza mienendo ya utandawazi wa vyombo vya habari na mawasiliano na athari zake kwa jamii. 

Prisca Kowa
Afisa Mwandamizi - Ushirikiano wa Kimkakati na Utekelezaji
Contact Info
Education
Shahada ya Uzamili ya Utafiti na Sera za Umma , Chuo Kikuu Dar es Salaam, Tanzania
Shahada ya kwanza ya Sosholojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Prisca Kowa anafanya kazi Policy Forum kama Afisa Mwandamizi - Ushirikiano wa Kimkakati na Utekelezaji. Kabla ya kupata nafasi hiyo alifanya kazi kama Msaidizi wa Programu ya Kuongeza Uwezo na baadaye Afisa Programu Tawala Serikali za Mitaa. Kabla ya kujiunga na PF, Prisca alifanya kazi CARE International na Aga Khan Foundation. Katika mashirika yote mawili alifanya kazi katika miradi ya maendeleo ya jamii. Prisca ana uzoefu mkubwa wa masuala yanayohusiana na serikali za mitaa na jinsi inavyosimamiwa nchini Tanzania. Kitaaluma, ana Shahada ya Uzamili ya Utafiti: Sera za Umma na Shahada ya kwanza ya Sosholojia zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Yeye pia ni mhitmu wa Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini. 

Haitham Kichwabuta
Afisa Prohramu - Tathmini na Ufuatiliaji
Contact Info
Education
Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Miradi, Ufuatiliaji na Tathmini ya Afya, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili
Shahada ya Sayansi ya Mazingira na Usimamizi, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Haitham Kichwabuta amejiunga na Policy Forum kama Afisa wa Tathmini, Ufuatiliaji na Kujifunza (MEL) anayehusika na kuongoza shughuli za MEL katika shirika. Kwa zaidi ya miaka minne, Haitham amekuwa akifanya kazi katika masuala ya Ufuatiliaji na Tathmini katika sekta za mazingira, kilimo na afya ya umma. Ana ujuzi wa kina na uelewa wa usimamizi wa miradi, ufuatiliaji na tathmini na anauzoefu wa kuripoti kwa wafadhili tofauti wakati akifanya kazi na Oxfam nchini Tanzania na kampuni ya ushauri kabla ya kujiunga na PF. Haitham ana shahada ya Sayansi ya Mazingira na Usimamizi kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo na Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Miradi, Ufuatiliaji na Tathmini ya Afya inayotolewa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili.

Hellen Massawe
Afisa Programu- Uchambuzi wa Sera
Contact Info
Education
Shahada ya Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Mafunzo ya  Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini.

Hellen Massawe alijiunga na Policy Forum kama Msaidizi wa Programu - Bajeti na Uchambuzi wa Sera. Yeye ni mhitimu katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam katika Shahada ya Sheria. NI mhitimu wa mazoezi ya kisheria kutoka Shule ya Sheria ya Tanzania. Hellen ana historia nzuri katika masuala ya kisheria ambayo ni muhimu katika masuiala ya sera.

Iman Khatib
Afisa Programu - Uchechemuzi & Ushirikishaji na JInsia
Contact Info
Education
Shahada ya Sheria, Chuo Kikuu cha Tumaini, Tanzania
Mafunzo ya  Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini.

Iman Hatibu alijiunga na Policy Forum mwaka 2017 kama Msaidizi wa Programu: Uchechemuzi na Ushirikishaji. Iman ana elimu ya sheria ambayo alimaliza masomo yake ya shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Tumaini. Aliwahi kufanya kazi na UNA Tanzania (mwanachama wa Policy Forum) katika masuala ya maendeleo kama msimamizi wa programu ya mafunzo. Iman alipata mafunzo kutoka kwa Wakala wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Uswidi (SIDA) huko Härnösand, Uswidi. Amefanya kazi katika sekta ya mawasiliano na uchechemuzi wa maendeleo endelevu, haki za binadamu, utawala bora, demokrasia, amani na usalama. Iman huleta uzoefu mwingi katika kutetea maswala ya haki za binadamu, baada ya kushiriki katika harakati za haki za binadamu tangu umri mdogo.

Amani Ndoyella
Msaidizi wa Ofisi na Utawala
Contact Info
Education
Astashahada ya Usimamizi, Bodi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Vifaa (NBMM), Dar es Salaam, Tanzania

Amani Ndoyella alijiunga na Policy Forum mnamo mwaka 2004 baada ya kumaliza mafunzo ya Astashahada ya Usimamizi wa Vifaa (NBMM). Amani ni kati ya waajiriwa wa kwanza kabisa wa Policy Forum na kwa sasa ndiye mwajiriwa aliyedumu kwa muda mrefu Policy Forum. Amani anasimamia masuala yote ya ofisi, vifaa, taarifa za ofisi, orodha na habari za wanachama wa mtandao.

Rashid Kulewa
Dereva
Contact Info
Education
Astashahada ya Mafunzo ya Kompyuta, Kituo cha Mafunzo (ICL), Dar es Salaam, Tanzania

Rashid Kulewa alijiunga na Policy Forum mnamo mwaka 2010, Alimaliza kozi yake ya astashahada katika masomo ya kompyuta katika Kituo cha Mafunzo cha ICL. Rashid amefanya kazi ya udereva na afisa msaidizi usimamizi wa vifaa na mashirika tofauti kama vile FHI na Axios Foundation.