Skip to main content
Semkae Kilonzo
Mkurugenzi Mtendaji
Contact Info
Education
Digrii ya Uzamili ya Uandishi wa Habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Uingereza
Mafuzo ya habari, Dublin, Ireland
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Semkae Kilonzo ni Mkurugenzi Mtendaji wa Policy Forum, mtandao wa mashirika 62 ya asasi za kiraia za Tanzania unaolenga kuimarisha utawala bora na matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma kwa kujenga uwezo wa wadau wa kiraia kushawishi na kufuatilia utekelezaji wa sera, pamoja na kuimarisha mwitikio wa serikali kwa ajenda ya utetezi ya asasi za kiraia inayohusu matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Semkae ana uzoefu mkubwa katika kazi za utetezi wa sera akiwa na asasi za kiraia nchini Tanzania, na ana shauku ya kupambana na mtiririko haramu wa fedha hususan katika sekta ya uziduaji, pamoja na kuhakikisha usimamizi wa mapato yatokanayo na rasilimali asilia unawanufaisha wananchi kupitia ushirikiano wa kimkakati kati ya serikali, sekta binafsi na jamii.

Semkae ana shahada ya uzamili (Masters) katika Uandishi wa Habari na Masomo ya Vyombo vya Habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Uingereza, na alipata mafunzo yake ya awali ya uandishi wa habari nchini Ireland (Dublin) na katika Chuo cha Uandishi wa Habari cha Tanzania. Pia ni mhitimu wa kozi ya Misingi ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji wa Huduma za Umma (Fundamentals of Social Accountability Monitoring Course) ya Public Service Accountability Monitor (PSAM) katika Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini.

Aidha, Semkae ni mwanzilishi mwenza na mjumbe wa Bodi ya Hakirasilimali, jukwaa la asasi za kiraia linalofanya kazi kwenye masuala ya kimkakati yanayohusu uchimbaji wa madini, mafuta na gesi nchini Tanzania

Gibons Mwabukusi
Meneja- Fedha & Utawala
Contact Info
Education
Stashahada ya Uhasibu, Taasisi ya Uhasibu Tanzania
CPA

Gibons Mwabukusi alijiunga na Policy Forum mwaka 2010 kama Afisa Fedha na Utawala. Kabla ya kujiunga na PF, Gibons alifanya kazi na AZAKI mbalimbali kama Afisa Fedha na Utawala. Ana Stashada ya Uhasibu kutoka Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) na pia ana CPA.

Richard Angelo
Meneja - Tawala Serikali za Mitaa
Contact Info
Education
Shahada ya Sanaa ya Sosholojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania
Mafunzo ya  Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini.

Richard Angelo ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo alisoma Shahada ya Sanaa katika Sosholojia na kuhitimu mnamo 2006, Hapo awali alifanya kazi HakiElimu na baadaye kama mshauri katika kitengo cha habari. Alijiunga na Policy Forum mwaka 2008 kama Msaidizi wa Programu- Vyombo vya Habari, Mawasiliano na Uchechemuzi na kwa sasa ni Meneja wa Tawaka Serikali za Mitaa. Yeye pia ni mhitimu wa mafunzo ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini na pia amehudhuria pia Mafunzo ya Wakufunzi (ToT) ya SAM.

Elinami John
Meneja - Uchechemuzi & Ushirikishaji
Contact Info
Education
Shahada ya Uzamili katika Vyombo vya Habari na Mawasiliano, Chuo Kikuu cha Karlstad, Uswidi
Shahada ya Sanaa katika Mahusiano ya Umma na Matangazo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Elinami John alijiunga na Policy Forum mnamo Septemba, 2016. Hapo awali alifanya kazi kama afisa programu anayesimamia upatikanaji wa taarifa na uhuru wa vyombo vya habari katika Baraza la Habari Tanzania (MCT). Alimaliza shahada yake ya kwanza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania. Ana shahada ya Uzamili katika Vyombo vya Habari na Mawasiliano kutoka Chuo Kikuu cha Karlstad, Uswidi. Anapenda zaidi kuchunguza mienendo ya utandawazi wa vyombo vya habari na mawasiliano na athari zake kwa jamii. 

Prisca Kowa
Afisa Mwandamizi - Ushirikiano wa Kimkakati na Utekelezaji
Contact Info
Education
Shahada ya Uzamili ya Utafiti na Sera za Umma , Chuo Kikuu Dar es Salaam, Tanzania
Shahada ya kwanza ya Sosholojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Prisca Kowa anafanya kazi Policy Forum kama Afisa Mwandamizi - Ushirikiano wa Kimkakati na Utekelezaji. Kabla ya kupata nafasi hiyo alifanya kazi kama Msaidizi wa Programu ya Kuongeza Uwezo na baadaye Afisa Programu Tawala Serikali za Mitaa. Kabla ya kujiunga na PF, Prisca alifanya kazi CARE International na Aga Khan Foundation. Katika mashirika yote mawili alifanya kazi katika miradi ya maendeleo ya jamii. Prisca ana uzoefu mkubwa wa masuala yanayohusiana na serikali za mitaa na jinsi inavyosimamiwa nchini Tanzania. Kitaaluma, ana Shahada ya Uzamili ya Utafiti: Sera za Umma na Shahada ya kwanza ya Sosholojia zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Yeye pia ni mhitmu wa Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini. 

Amani Ndoyella
Msaidizi wa Ofisi na Utawala
Contact Info
Education
Astashahada ya Usimamizi, Bodi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Vifaa (NBMM), Dar es Salaam, Tanzania

Amani Ndoyella alijiunga na Policy Forum mnamo mwaka 2004 baada ya kumaliza mafunzo ya Astashahada ya Usimamizi wa Vifaa (NBMM). Amani ni kati ya waajiriwa wa kwanza kabisa wa Policy Forum na kwa sasa ndiye mwajiriwa aliyedumu kwa muda mrefu Policy Forum. Amani anasimamia masuala yote ya ofisi, vifaa, taarifa za ofisi, orodha na habari za wanachama wa mtandao.

Rashid Kulewa
Dereva
Contact Info
Education
Astashahada ya Mafunzo ya Kompyuta, Kituo cha Mafunzo (ICL), Dar es Salaam, Tanzania

Rashid Kulewa alijiunga na Policy Forum mnamo mwaka 2010, Alimaliza kozi yake ya astashahada katika masomo ya kompyuta katika Kituo cha Mafunzo cha ICL. Rashid amefanya kazi ya udereva na afisa msaidizi usimamizi wa vifaa na mashirika tofauti kama vile FHI na Axios Foundation.