Skip to main content
Semkae Kilonzo
Katibu wa Bodi
Contact Info
+255 782 317 434
coordinator@policyforum.or.tz
Education
Shahada ya Uzamili ya Uandishi na Vyombo Habari, Chuo Kikuu cha Cardiff, UK
Mafunzo ya Habari, Dublin, Ireland
Mafunzo ya Msingi ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini

Semkae Kilonzo alianza kazi Policy Forum mwaka 2007 kama mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Uchechemuzi anayehusika na vyombo vya habari, ikiwa ni shauku ya mtandao kuona taarifa zinazohusiana na uchambuzi wa sera zikisambazwa kwa watunga sera, asasi za kiraia na umma kwa jumla. Akiwa kama mratibu na baadaye kama Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao amekuwa akiongoza Sekretarieti  katika majukumu ya kila siku ya kiofisi. Semkae pia ni mjumbe wa Kamati  ya Uwazi wa Bajeti, Uwajibikaji na Ushirikishwaji Global Movement for Budget Transparency, Accountability and Participation (BTAP).

Semkae ana digrii ya Uzamili ya Uandishi wa Habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Uingereza na pia amepata mafunzo kuhusu vyombo vya Habari, Dublin Ireland na pia katika  Shule ya Uandishi wa Habari Tanzania (TSJ). Semkae ni mhitumu wa mafunzo ya  Ufuatiliaji wa Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini. Semkae anapenda sana kuhamasisha ushiriki wa umma katika utengenezaji wa sera na matumizi ya rasilimali za umma yanayozingatia usawa.

Semkae hushiriki katika vikao vya Bodi ya Wakurugenzi kama Katibu wa Bodi.

We should be passionate about encouraging public participation in policy making and championing the equitable use of public resources