Skip to main content
Submitted by Web Master on 3 July 2018

Ufanisi wa mfumo wowote ule wa kukusanya kodi za majengo unahitaji ushirikiano imara kati ya Mamlaka ya Ukusanyaji wa Kodi na Halmashauri za Miji/Majiji. Aidha, ni budi kuwepo na mgawanyo ulio wazi na bayana wa majukumu na madaraka ya mamlaka hizo. Katika miaka kumi iliyopita mfumo wa kukusanya kodi ya majengo katika Tanzania umekuwa ukibadilika mara kwa mara kati ya mfumo wa kugatua madaraka kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mfumo wa kukusanya kodi hiyo moja kwa moja kwa kutumia Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi ya Serikaali Kuu. Andiko hili linachambua uzoefu uliopatikana kutokana na mifumo hiyo miwili ya ukusanyaji wa kodi ya majengo. Soma zaidi