Skip to main content
Submitted by Web Master on 5 March 2018

Mwanzoni mwa mwaka 2016, Serikali ilizindua FYDP II, kwa lengo la kurekebisha mapungufu ya FYDP I na kutoa mpango makini wakati Tanzania inapoanza kuelekea katika maendeleo ya viwanda katika miaka mitano ijayo (2016 – 2021).

Katika kufanya marejeo ya FYDP I, serikali ilitambua kuwa mpango wa awali ulishindwa kufanikisha malengo yake mengi. Wakati Serikali imedhamiria kuwa ukuzaji wa viwanda ni kipaumbele katika miaka mitano ijayo, mapungufu ndani ya mpango unaweza kufanya nchi ishindwe kwa mara nyingine tena kama masuala yaliyojitokeza hayajafanyiwa kazi vya kutosha.

Majadiliano yaliyopita kati ya Serikali na mashirika binafsi yaliyofanyika mwaka 2016, yaliyolenga kufanyia kazi changamoto na masuala ndani ya FYDP II hayajaleta matokeo yaliyokusudiwa. Ili Tanzania ifanikiwe, mbinu mpya na mawazo mapya yanahitajika haraka. Utekelezaji wa ufanisi wa FYDP II utahitaji uelewa wa ndani wa kwa nini majaribio ya nyuma ya kuimarisha viwanda yalishindwa na kuchukua hatua kuhakikisha kwamba makosa ya nyuma hayarudiwi. Soma zaidi