
Israel Ilunde ni mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa The Youth Partnership Countrywide (YPC), Shirika la Kiraia linalofanya kazi katika kuwawezesha vijana wa kike na wa kiume katika masuala ya uraia na uchumi kupitia mafunzo katika utawala na ujasiriamali, midahalo, uhamasishaji, na uzoefu wa kazi za hiari. Bwana Ilunde kama Mtendaji Mkuu wa YPC amefanikisha na kusimamia kwa kina na kwa ujumla kubuni miradi, mipango, uhamasishaji wa rasilimali, utekelezaji, ufuatiliaji, ujifunzaji, na tathmini ya shughuli zote za YPC pamoja na kujenga ushirikiano na miradi ya pamoja.