
Fatma ni Mkurugenzi wa Fedha aliye na uzoefu wa zaidi ya miaka 5 kwenye tasnia ya masuala ya fedha hasa kwenye sekta ya elimu kwa njia ya mtandao. Anaujuzi wa mipango katika biashara, mikakati, utafutaji fedha, bajeti, na usimamizi wa rasilimali fedha na watu. Fatma ana ujuzi wa uongozi, mawasiliano ya umma, usimamizi wa miradi na masuala ya kijamii
Fatma alizaliwa na kukulia nchini Tanzania; anapendelea kuona sekta ya elimu kama nyenzo ya kutokomeza umasikini barani Afrika na anaamini vijana wana nguvu na uwezo wa kuleta mabadiliko chanya ulimwenguni. Tangu akiwa mtoto, Fatma amekuwa akishiriki katika kuwawezesha watoto, vijana na wanawake.