Skip to main content
Christina Kamili Ruhinda
Mwenyekiti wa Bodi
Contact Info
info@tanlap.or.tz
Education
Shahada ya Uzamili ya Sayansi ya Uongozi na Utawala, Chuo Kikuu cha Jomo Kenyatta, Kenya

Bi Christina Kamili Ruhinda ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Watoa Huduma za Kisheria Tanzania (TANLAP). Pia ni Mwenyekiti wa Songera - Songera - Mississippi Organization (SOMI), Tangible Initiative for Local Development (TIFLD), Tanzania Youth Inspiration Organization (TaYIO) na Door of Hope to Women and Youth Tanzania ( DHWYT)pia ni Mwanachama wa Kamati ya Usimamizi wa Kesi  iliyoanzishwa chini ya Waraka wa Jaji Mkuu Namba 5 ya 2018, ni Mwanachama mwanzilishi wa Mtandao wa Kikanda wa Afrika Mashariki wa Watendaji Walio na Wasio wa Serikali, ni Mwanachama wa Timu ya Msaada wa Kisheria ya Kitaifa ya Wizara ya Katiba na Sheria, mwanachama wa Mtandao wa Umoja wa wa Wanawake wa Kiafrika wa Kuzuia Migogoro na Usuluhishi (FemWise-Africa).

Bi Ruhinda ana uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika masuala ya Sheria, Haki za Binadamu, Jinsia, Uongozi, Uangalizi wa Uchaguzi, Mitandao, Usimamizi wa Programu na Ukuzaji wa Uwezo. Pamoja na mambo mengine, amekuwa akishiriki katika utambuzi wa maswala ambayo yameathiri upatikanaji wa haki nchini Tanzania.

Making policies work for people in Tanzania