Skip to main content
Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum hivi karibuni walishiriki katika siku ya kumkumbuka Kanumba , Mtengeneza filamu na Muigizaji ambaye alifanya  kazi na mtandao huo kuigiza dhana ya ufuatiliaji wa uwajibikaji kwa jamii (SAM).


Dhana(script) iliyotengenezwa kwa pamoja na Policy Forum, watungaji na Kanumba zilipelekea utengenezaji wa filamu ya " Kijiji cha tambua Haki ", filamu ambayo inaonyesha mapambano ya kila siku ya wanajamii wa kijijini katika kupigania uwajibikaji wa serikali za mitaa.

Policy Forum aliamua kutumia filamu ili kuweza  kutoa ujumbe kwamba jamii zina nafasi ya kucheza katika kuboresha utoaji wa huduma na kufanya viongozi wao wawajibike kwa ajili ya matumizi ya fedha za umma.

"Katika nchi ambapo wanaume na wanawake wengi wanapendelea kuangalia sinema kuliko kusoma, uwezo wa kuelimisha kupitia burudani ni mkubwa sana ," alisema Samwel Stanley, kutoka shirika la Youth Partnership Countrywide ( YPC ), mwanachama wa Policy Forum ambaye aliwakilisha Bodi ya Policy Forum wakati wa tukio hilo ambao lilifanyika katika ukumbi wa Dar Live, Mbagala.

Kwa makadirio ya sinema mpya kumi za bajeti ya chini huzalishwa kila wiki na sita kuachiwa huru katika soko, mbinu hii kweli huonekana kama njia bora ya kufikia idadi kubwa ya watu kwa gharama nafuu.

" Ufuatiliaji wa uwajibikaji kwa jamii (SAM) inaweza kuwa dhana ngumu kama inavyofundishwa katika chumba cha semina , lakini kiini chake ni kuwawezesha wananchi waweze  kudai udhibisho na uhalalisho kutoka kwa viongozi wao kwa matendo yao na kuwafanya wawajibike kwa maamuzi yao ni kitu kikubwa ambacho filamu hii inajaribu kuonyesha, "Stanley alisema.

" Policy Forum walifadhili kwa sehemu tukio hili kama njia ya kuonyesha shukrani kwa ajili ya ushirikiano waliokuwa nao na marehemu Kanumba na kama jitihada za kuendelea kufikia nje kwa Watanzania na kuwaelimisha juu ya haki na wajibu wao katika kukuza uwajibikaji katika nchi," alisema, akiongeza kuwa Policy Forum itaendelea kuchukua faraja kwamba mtandao unamuona Steven Kanumba ,  kama kijana mtaalamu na mfano wa kuigwa katika jamii.
 

Kuona promo ya filamu hiyo bofya hapa chini:

https://www.youtube.com/watch?v=aaCYVfAv7sM